Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka
Showing posts with label Nuruthelight house hunting. Show all posts
Showing posts with label Nuruthelight house hunting. Show all posts

Tuesday, May 2, 2017

THEY DON!T WANT US TO BE GREAT POINT BLANK PERIOD!!!

















 huyo kwenye simu tulikuwa nae kimwili tyuu..,


 A Lil Milkshake never hurt nobody.,.,

 Yummy

Wakipiga kelele ongeza spidi.
Wakipiga kelele ongeza juhudi.
Wakipiga kelele kaza mwendo.
Wakipiga kelele kataa uwoga na ongeza ushujaa.
Kelele zisiwe kisingizio wewe kutofanya.,
Kelele zisiwe sababu ya wewe kusema haiwezekani kwani mifano hai ipo na unaiona.
Kelele zisikufanye ukatike moyo bali zigeuze na kuziona kama uhamasishaji.
Kelele zipo kama ukumbusho kuwa unakaribia malengo yako kwani ulisikia wapi mvivu akipigiwa kelele?
Kujitambua si kitu huja tu bali ni safari na wengine bado hawajaanza hiyo safari so cha msingi ni kuelewa kuwa unachokiona wewe si kile anakiona mwenzako.
Wote mnaweza kusoma kitabu kimoja ila perception Zenu zikawa tofauti.
Kuna watu kazi yao ni kuamka na kutukana wengine kila kukicha lakin kwavile kwake yeye anajiona yuko sawa je wewe ni nani kumwambia hayuko njia sahihi?
As long as people watakuwa na jukwaa kwa kutukana au wakifanya mabaya juu ya watu basi kamwe hawawezi jiona kuwa wanakosea na Sometimes wallopo jukwaani na kutizama na kushangilia hao ndio wabaya zaidi.
Kuna wasiofaham na kujua uchungu wa mwenzao mpaka yawakute.,
Kuna wanaojua uchungu na maumivu ya wenzao na bado wanafurahia kwani hiyo ndio faraja yao.
Katika maisha muogope sana mtu ambae ameshagive up na maisha yake kwani hana lolote la kuhofu tena au kuogopa tena meaning anaweza kufanya chochote kwa yoyote mda wowote.
Jaribu kuona maisha yako mbali na sio ya leo tuu basi utakuwa motivated sana trust me on this.
Katika maisha Jua kwamba Wewe ndio Mchoraji wa ramani na safari ya Maisha Yako so Chora ramani ambayo itakutangaza wewe Vyema si kwako tu bali hata kwa wale waliokuzunguka,Nimemaliza.com!!!


Thursday, April 6, 2017

HE SAID SEEK AND YOU SHALL FIND SIMPLY BECAUSE NOTHING IS FOR FREE!!!





















Bila kujaribu huwezi kusema haiwezekani.
Bila kuthubutu huwezi kusema haiwezekani.
Bila nia kuwepo na wewe kutenda huwezi kusema haiwezekani.
Bila kuwa jasiri na kuwa na subra huwezi kusema haiwezekani.
Bila kuwa consistent,disciplined na msimamo hauwezi sema haiwezekani.
Bila kuwa na imani,hope na kuwa tayari kisaikolojia hauwezi sema haiwezekani.

Neno haiwezekani ni la Wavivu au watu waliokata TAMAA.
Neno haiwezekani ni faraja kwa wenye chuki kwani wao walishajiamulia kuwa haiwezekani.
Neno haiwezekani ni kwawale walijaribu na kufeli na kukata tamaa baadae kwani walipaswa kujaribu tena au inawezekana kuwa hawakuwa na elimu nacho au the timing haikuwa sahihi.
Neno haiwezekani ni kwa wale watu amber wanaridhika upesi sana kwenye maisha yao.

Kwenye maisha yenu watu waliowazunguka ni wengi sana so kama wewe utafuata wale wa haiwezekani basi naam nawewe utakuwa kundini lakini ukiamua kuchukua njia yako mwenyewe kwa kile unaamini kinawezekana basi utafanikiwa.
Sio kwamba kuwa tajiri na hela nyingi ndio maana ya mafanikio kwani mafanikio yana sura nyingi sana hicho ni kitu mnatakiwa muelewe na mkielewa hilo basi formula ya maisha haitowasumbua at all.
Mfano Kuwezekana inaweza kuwa mtu aliacha shule udogoni but akarudi ukubwani kwani ukubwani ndio alikuwa tayari kusoma.
So wakati unalitizama neno Haiwezekani lijadili,litizame kwa jicho la tatu na liulize maswali kuwa je kwanini Haiwezekani na ukishapata jibu anza kulifanyia kazi,Nimemaliza.com!!