Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Wednesday, October 7, 2015

MUNGU AMLAZE PEMA MAMA SHERIA NGOWI NA HAKI NGOWI!!!


RATIBA YA MAZISHI YA MAREHEMU MARY THOMAS NGOWI.

Familia ya Marehemu Mzee Thomas Kishari Ngowi kutoka Tabata,Segerea, inasikitika kutangaza kifo cha Mpendwa wao, Mama Mary Thomas Ngowi kilichotokea Jumatatu,05 Oktoba 2015 ktk Hospital ya Tabata General alipolazwa baada ya kuugua kwa muda mfupi. -Msiba upo Nyumbani kwa Marehemu Tabata,Segerea "Kwa Mama Ngowi". Ratiba ya Mazishi ni kama ifuatavyo;
*Leo Jumanne,07 Oktoba 2015
Saa 9 Jioni - Mwili wa Marehemu kuwasili Nyumbani kwake Tabata-Segerea. *Saa 9-10 jioni - Misa/Ibada ya kumuombea marehemu itafanyika hapo hapo nyumbani kwake. *Saa 10-11 jioni-Heshima za mwisho zitaanza kutolewa na kufuatia na sala na maombi mbalimbali yataendelea

Alhamisi,08 Oktoba 2015
*Saa 4-5 Asubuhi - Misa Takatifu
Itafanyika katika Kanisa Kuu la Mt.Yoseph (St.Joseph Cathedral-Mjini). *Saa 6-7 Mchana - Heshima za mwisho kwa Marehemu zitaanza kutolewa. *Saa 8-9 Mchana Safari ya kuusafirisha mwili wa marehemu kuelekea Moshi itaanza.

Ijumaa,09 Oktoba 2015
*Saa 2-3 Asubuhi -Mwili wa marehemu utawasili Kijijini kwake Old Moshi,Tela Mande. *Saa 7 Mchana Misa Takatifu
Itafanyika hapohapo Old Moshi,Tella Mande katika mkoa wa Kilimanjaro. *Saa 7-9 Mchana - Heshima za mwisho kwa Marehemu zitaanza kutolewa. *Saa 10 Jioni - Shughuli za Mazishi zitaanza.

Bwana alitoa na Bwana ametwaa, jina la Bwana lihimidiwe - Amen🙏

No comments: