Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Monday, July 20, 2015

AND THE SAGA CONTINUES!!!



Tuki-support mtu ndio kama hivi matokeo yake mtu anatumia baadae kukudhalilisha. Hii video aliyo-post kwanza ni #TBT kama sijakosea mwaka jana mwishoni nilikuwa sehemu na my friends @bikira_wa_kisukumaakani-record na kumtumia@diamondplatnumz bila mimi kujua. Kiukweli sijui kwanini walifanya hivyo. Nikaja kujua baadae sana na nikaona sio big deal cause kila mtu anapenda mziki na sio dhambi kucheza mziki wowote uupendao. Ila kitendo cha@diamondplatnumz kwenda kuitafuta huko ilikokuwa hii video clip na kui-post leo najiuliza maswali mengi 1, anataka ionekana kama nilikuwa nashangilia ushindi wake? Which is not bad hakuna ubaya hapo kama unaamini ushindi wake ni sifa kwa taifa ila 2, Kwanini a-post na caption ya Na Bado Mtanyooka? Ili amkomoe nani? Au kwasababu niko karibu saaana na @alikibaofficialanatafuta kutuchonganisha? Ili iweje? Mimi I believe life goes on na kila mtu ana uhuru wa kumpenda au kuwa karibu na yule apendaye na kum-support ndio maana hata mimi nimekuacha na your new life 3, Pengine ni kweli anaendeleza zile hulka zake za kudhalilisha wanaweke aliokuwa nao waonekane sio kitu just because hawako na diamond platnumz chibu dangote. Which to me is just dead wrong. @diamondplatnumz hizi sio tabia tunazozitegemea kwa mtu anayejisema anakomboa mziki wa Tanzania sio kwa kuweka visasi na fitna zako wazi wazi hivi. Unatu fanya tukose imani nawewe zaidi na tunaogopa ku-support cause hukawi kutugeuka. Kuwa tofauti basi, onyesha mfano kwamba kweli hupendi beef unapenda mziki wa Tanzania uendelee ila kwa ulichoki-post unaonyesha wazi UNA visirani na hutaki mema unatafuta drama, kiki, vurugu unataka kila siku uwe wewe tu ambazo kiukweli mimi binafsi siziwezi utaendelea kushinda wewe tu katika hilo na sitashindana nawewe katika hilo kwasababu siwezi nawewe unajua kama ulivyoniimba mimi mpole, sinaga maneno ( ila kwenye kazi ndio nakuwa mkali kama pilipili ). Ila ungetumia busara kidogo. Just move ON kiroho safi. Naomba pia nitumie fursa hii kukupongeza kwa tuzo yako ya MTV ila@babutale hata wewe ndugu yangu? Is this how tunaendeleza so called uzalendo? Inshallah Kheri lakini yote maisha wanyonge sisi iko siku Mungu atatunyanyua. ��


haya ndio majibu ya Diamond kuhusu video aliyoipost na kile alichokiandika Jokate:
“unajua kwanza nimecheka afu nimeskitishwa kwasababu nimeambiwa, sijasoma nimeambiwa kuna post ameandika amezungumzia vitu vingi… Yeye kacheza kama fan wa nyimbo yangu, na mimi nimempost kama fan wangu, ile caption yangu sijamuandika jina kwanini achukulie vibaya? Ukiona mtu anajishuku ukiona hivyo kuna namna nyuma. Mbona mi napost watu wengi tu, tena naandika caption zangu za vituko vituko manake mimi nina caption za vituko, mi ni mswahili nimezaliwa Tandale nimekulia Tandale na Tandale ndio kumenifanya leo niwe hapa nilipo…kwahiyo nina caption zangu za uswahili kwasababu uswahili ndio umenikuza…siziachi kuziandika mbona naziandikaga katika caption nyingi nyingi kwanini kwake yeye tu aione tatizo, kwani kuna ubaya gani mi kuandika mtanyooka tu kama yeye haimuhusu ina maana labda kuna kitu kinamuhusu.”
Diamond aliendelea: “Nikaambiwa pia amezungumza kwamba ndio maana wanaogopa kusapoti wasanii watanzania kwasababu akisapoti wanadhalilishwa, yeye mimi mpaka nimeenda kuchukua tuzo hii amenisapoti nini? Alipost hata post moja kusema mpigie kura Diamond, afu leo anajishaua eti kanisapoti, kasapoti nini eti kutoa hongera mi nimeshinda tuzo, eti ooh hongera kwa tuzo by the way, angepost kuhamasisha watu wapige kura ili ushindi uje nyumbani, lakini kwa chuki alizojazwa zisizo na sababu na roho mbaya alowekwa na watu imemfanya ashindwe hata kunipost na kutengeneza chuki za chini chini kwa kudhani wakiwapigia kura Wanigeria mi ntakosa tuzo…Mungu alivyolaani mi nimeshinda, afu anajifanya anatoa hongera eti wanasapoti muziki wa kiTanzania, utanisapoti nini, lini umenisapoti, au baada ya kuona tuzo imekuja ndo unajifanya kutoa hongera, tuacheni unafiki.”

6 comments:

Anonymous said...

Ivi mtu anaepeperusha bendera ya Taifa ndo upeo wake wa kuongea huu?? Eish! this Diamond dude I give up ooh. Mchemsho.com

Anonymous said...

Nuru, I would like to hear your side of view on this issue? Please

Anonymous said...

to each his own!!

Anonymous said...

Hahaha! Mie naona Diamond angeeachaa kujibizana na watu jamani! Apige kimyaaaaaa watanyoooka wenyeweeeee Tu mbona!!! Maaana huyu Jokate alikuwa Ex-wakeeee sasa naona badoo wanapendana kidogo maana wooote mapovu yamewatokaaaaa sanaaaa tu! Mie Ningekuwa mshauri wa Diamond ningemshauri apige kimyaaaa kwa yoyote anaye piga blah blah zisizo za maendeleooooo!!!! Hakuna hajaa wala sababu ya Diamond kujishushia hadhiii kwa kubishana na watu vitu hovyooooo! Kwanza Hata ku discuss hiyo video ya huyo mwanadada akicheza mziki wake ni kujishusha tu hakuwa na hajaaaaa ya kupost video na kuweka " mtanyooka" no! No! No! Diamond Tafadhali wacha mabishano ya kijinga ..... ( Maoni yangu) ( my opinion)🙊🙈🙉

Anonymous said...

Ndio kashaipeperusha na Tuzo karudi nayo. Tuwaachi wenyewe wanajuana.

sinyora said...

Hawa wanawake wao ndo wanafki jamani,na diamond ana moyo pia!! muacheni tu awajibu bwana.. wasimpande kichwani!!! hakuna hata aliotoa support ya kumpigia kura,acha awapake!! wanamuanzaga sometimes bana