Flora wewe ni JEMBE saluti kwako!
STRONG WOMAN
Yaani upepo uliokupitia ni upepo mkali sana hasa kwa jamii zetu ambazo Mwanamke anatakiwa anyamaze kwa lolote linalomkuta kwenye NDOA yake. Hata kama yupo kwenye hatari ya kupoteza roho yake jamii itamuona mkosaji tuu!!! Lakini umeweza kuhimili na kuendelea na kazi kama kawa kama dawa....
Umechambwa vya kutosha na ukahukumiwa kisawasawa, badala ya kusubiri Hukumu ya Mahakama. Wala kuangalia mlalamikaji wa hiyo kesi kama na yeye ana Haki au la! Kama ni kesi ya kutunga pia itadhihirika siku za mbele Mahakamani... hapa Flora na Mbasha mnajua kilichotokea na kinachoendelea.. sipasemei sana nsije tukanwa kama nilivyoshukiwa...
HOJA YANGU
Leo umenisapraiz sana kukuona ukiendelea na Huduma kama vile hakuna kilichotokea ukiwa Mwanza karibu na ccm kirumba kwa siku tatu. Leo ndo umemaliza Huduma!! Wewe ni zaidi ya Super Woman dada Flora. Kwa hilo Wanawake wengi tunajifunza kuwa Maishani kuna mambo mengi sana yanatokea mengine yanaumiza sana sana ila jaijalishi, kikubwa tunapaswa kujifunza kukabiliana na changamoto za aina yeyote ile... kwa somo hilo nakushukuru sana na nakupongeza sana....
Hakuna ajuae ukweli wa yaliyoipata nyumba yako zaidi ya nyinyi wenyewe na Mungu wenu pekee. Wengine wote tunapiga kelele tuu...ila pia ninachokiona ni kwamba Watu wengi sana wanaenda kuomba watu wakiharibikiwa kuliko mafanikio ya watu zaidi. Siku watakayokusapoti ni siku utakayomaliza safari ya hapa duniani ndo rip zitakuja mabilioni... usiogope wanaokuhukumu leo kwani nao ni binadamu tuu kama wewe na mimi...
RAI YANGU
Wanawake tukiendekeza tabia za kukaa kimya dhidi ya maovu na unyanyasaji na ukatili tufanyiwayo, hali itazidi kuwa mbaya zaidi huku tuendako. Ni wajibu wako kujitendea Haki kwa kupaza sauti za kukemea au kupinga mambo yote machafu kwenye nyumba zetu...
KISA MKASA CHA KWELI
Kuna mama mmoja alikuja kwangu akilia kwa uchungu sana kwa sababu Mume wake alimwingizia mkono kwenye Sehemu zake za Siri(Ukeni) yaani mume akazamisha mkono!! Na amekuwa akiteseka sana kwenye hiyo Ndoa. Sasa cha ajabu yule mama hajawahi kumwambia ndugu yake wala hajawahi kushitaki popote!!! huyu mama anasubiri akatwe mguu au mkono ndo atoe tarifa???? Nimeligusia hili hapa kwa sababu ujumbe utafika! akina mama tusikae Kimya tena.
FLORA
Mungu wetu azidi kukutia Nguvu na familia yako usimame na uendelee na maisha na upepo huu uliopo upite salama maisha yaendelee kama zamani... Amen BY JOYCE KIRIA!!!

IMAGE AND CREDITS:WANAWAKELIVE.COM