Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Saturday, June 14, 2014

FROM SETH DE JESUS DE GIOVANNIE!!!






UNAMDANGANYA NANI???
Unajijua kabisa bado una tabia mbovu na hujasettle,unatafuta kabinti ka watu unatangaza ndoa unakaoa ili tu ukamgeuze kichaka cha kufichia umajnuni wako...Pete na Kiapo haina Auto-Eraser kubadili u-kimbito wako Overnight..Utaenda kumtesa tu binti wa watu wakati ulijua kabisa haukuwa tayari kutulia kufuata misingi ya Ndoa..
UNAMDANGANYA NANI??
Unajijua kabisa tabia zako mbovu na bado ni maharage ya Mbeya lakini umemkamata mjinga-mjinga flani kwa mbinu zako za Zena na Betina Ameingia Kingi ametangaza ndoa..Unajijua kabisa Unaekti na hauko tayari kwa Ndoa ila kwa sababu umelipata fala ambalo halikujui vizuri..umeliektia kwa muda mfupi kakuweka ndani only to find wewe ni machepele tu mbele haikai nyuma haikai wakati mwenzio alikuoa AKIMAANISHA
Wengi tunaoa na kuolewa tukiwa HATUKO TAYARI..Kuna forces behind...Wengi umri unawakimbiza...Wengine Wazazi wanauliza sana...Wengine wamefosiwa na PATA MIMBA UOLEWE(PMU),lakini ile Decision haikutoka from deep within
Ukiolewa ili 'Uwapooze Wazazi' utafanikiwa Kuwapooza kwa muda mfupi lakini kwa sababu Tabia zako haziendani na Jukumu uliloliingia Ni Wazazi hawahawa waliokupush uolewe watasema "TUMECHOKA KULETEWA KESI NA MMEO KILA SIKU"
Bata ni Bata tu,Hata akila mawe lazima ataharisha tu

No comments: