Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka
Showing posts with label HUSSEIN RAMADHANI. Show all posts
Showing posts with label HUSSEIN RAMADHANI. Show all posts

Tuesday, November 27, 2012

CHANZO CHA KIFO CHA MAREHEMU HUSSEIN RAMADHANI A.K.A SHARO MILLIONEA!!

HIS LAST TWEET..,
THE CAR HE DROVE!!
Habari za uhakika kuhusiana na chanzo cha kifo cha msanii Hussein Ramadhan a.k.an Sharo milionea ni kwamba gari yake aina ya Toyota harrier ilipata pancha tairi la upande wa kulia na kukosa mwelekeo kisha ikaacha njia na kuelekea mtaroni lakini ule mtalo haukuizuru sana gari hiyo ikaruka na kuingia katika shamba la maindi.
 Kitu kilichoshangaza wengi ni sehemu ambayo si hatarishi sana kiudereva sababu iko tambarare na kona si kali eneo hilo. 
 Chanzo cha habari kinaendelea kufafanua kuwa baada ya gari kuacha njia ilienda kugonga mti mkubwa na kuung'oa baada ya kuuchana katikati kutokana na gari ilivyokuwa mwendo kasi.
Mwili wa marehemu ulitupwa nje ya gari baada ya kugonga mti huo ambapo gari hiyo iliharibika vibaya kuanzia kwenye roof hadi vioo vyote kupasuka japo vizuizi vilifunguka lakinini havikusaidia.
 Baada ya kishindo kikubwa cha mlio wa pancha kilisikika kwa wakazi wa kijiji hiko na kuamua kujitokeza kujua nini kimejili pale na wakati wanafika hapakuwa na mwili wa marehemu katika  eneo la tukio,ndipo mama mmoja aligundua mwili wa msanii huyo mita chache kutoka gari ilipogonga mti na kuharibika vibaya.
 Mganga mkuu wa hospitali teule ya Muheza amesema kuwa chanzo cha kifo cha Sharo ni kubonyea kwa kichwa ikiambatana na majeraha yaliopo kichwani na sehemu ya mabega ndiyo yalipelekea msanii huyo kupoteza maisha papo hapo.
 Hata hivyo jeshi la polisi lilikuja masaa mawili baada ya kutokea ajali hiyo,ambapo gari la Tanesco ndilo lililotumika kuvuta gari hiyo hadi kituo cha polisi wilayani humo.
SOURCE:UNIQUE BLOG

I LIFE HUSSEIN RAMADHANI A.K.A SHARO MILLIONEA!!!

KWAKWELI SIJUI NIANZE WAPI MAANA MIDA YA SAA MBILI JANA USIKU TULIPATA HABARI KUWA SHARO MILIONEA AMEFARIKI DUNIA SIWEZI KUDESCRIBE THE FEELING AU SHOCK NILOPATA.TUNAUMBIWA TUSIMUULIZE MUNGU SWALI LA KWANINI ILA NILILIULIZA NA SI MARA MOJA TU BALI NYINGI.KWANZA NILISEMA SIAMINI NA SIKUAMINI MPAKA NILIPOONGEA NA MDOGO WANGU REY AMBAYE AKATHIBITISHA KWELI DADA NURU SHARO HATUKO NAO TENA DADA.AISEE WOTE TULILIA KWENYE SIMU.MPAKA SASA HIVI BADO SIAMINI.SHARO ALIKUWA ANAELEKEA TANGA KUMUONA MAMA YAKE NDIPO AKAPATA AJALI NA KUFARIKI.
KATIKA WASANII WA TASNIA YA FILAMU SHARO ALIKUWA NI MTU MCHESHI,MKARIMU,HANAGA MAMBO YA HATERISM KABISAAAAA,MPOLE NA ALIKUWA MTU WA AIBU SANA ILA MTU UKIMUONA KWENYE TV HUWEZI AMINI.KISANAA ALIKUWA AMEANZA KUPANDA SANA NA KUPATA MAFANIKIO NDIO MAANA NIKAMUULIZA MUNGU MBONA UNAMCHUKUA KIJANA WAKATI NDO KWANZA ANAANZA KULA MATUNDA YAKE BABA!!
WATU WENGI WALIMCHEKA MWANZONI NOT KNOWING HE WAS GOING TO MAKE AN IMPACT NA HATIMAYE SASA NAFSI ZAO ZINAWASUTA WAO.MSISUBIRI MPAKA WATU WAFE KUWAPA SIFA ZAO AU KUWASIFU KWA MEMA WANAYOKUTENDEA WEWE BINADAMU.SHARO AU HUSSEIN ALIKUWA NA NYOTA KALI SANAAA UKIPITA NAE MTAANI WATOTO NA WATU WAZIMAWANAKIMBILIA GARI KUMPA HI HALAFU MTU ANAKWAMBIA AHH USUPASTAA BONGO,,MSHINDWE NA MLEGEE KUKATA MIOYO YA WATU MAANA TUWAPE MOYO HAO WAJAO ILI WATANGAZE TAIFA LETU NA WATOTO WETU WAPATE ROLEMODELS WA KWAO.SINA ZAIDI ILA NAKUPENDA SANA SHARO NA MUNGU AKULAZE PEMA PEPONI,I LOVE YOU AND I WILL NEVER FORGET YOU MY LOVE!!