Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka
Showing posts with label EDUCATIONAL. Show all posts
Showing posts with label EDUCATIONAL. Show all posts

Wednesday, June 8, 2016

EDUCATIONAL:IGBO LANDING!!!


Kwenye video ya Beyonce kuna hii scene amesimama mstarini na hao wengine na chini mnaona picha ya watumwa ambao waliletwa marekani wakati wako njiani waligoma kwenye meli na kuiteka huku wakiimba nyimbo za kabila lao Igbo na kuifikisha kisiwani
Walipofika walisema ni bora wafe kuliko kuwa watumwa na kujipanga mstari mmoja huku wakiimba na kuelekea majini na mwisho wake kufa huku wamezama.
Hiki ni kitendo cha ushujaa kikionyesha kuwa bora tufe kuliko Utumwa na ilikuwa mwaka 1803 kisiwani St.Simon in Georgia Marekani.

 WEUSI TUMEPITIA MENGI SANA KIHISTORIA ILA BADO HAWAJITAMBUI AS PEOPLE OR AS A RACE,BADO TUNA SAFARI NDEFU MNO NA SIJUI KAMA ITAKUJA KUWA A REALITY BUT BADO WEUSI NI WATUMWA KWENYE DUNIA HII YA LEO
SIMPLE FACT KWAMBA AFRIKA INALISHA DUNIA NZIMA BALI NDIO BARA LENYEWE NJAA INAKUINGIA AKILINI KWELI?
AFRICA INA MADINI NA MENGINE MENGI ILA  NDIO BARA MASKINI,REALLY?
BADO TUNAPIGANA NA UTUMWA NA MAUWAJI KIKABILA NA KIDINI SISI WENYEWE KWA WENYEWE JE INAKUINGIA AKILINI KWELI,,
AHH MY AFRICA INDEED TUNASAFARI NDEFU NA ALOTULAANI SIJUI NI NANI!!

Monday, December 28, 2015

INSPIRATIONAL YET EDUCATIONAL!!



 THIS QUOTE IF PEOPLE UNDERSTOOD THAT WE ARE DIFFERENT,TALENTED IN DIFFERENT WAYS BUT WE ALL HAVE AN EQUAL OPPORTUNITY TO PERFECT THE TALENT THAT WE WERE BLESSED WITH,,THIS IS DEEP
KILA MTU ANA KIPAJI TOFAUTI NA TUNATOFAUTIANA KWENYE VIPAJI ILA KILA MTU ANA UWEZO  WA KUIBORESHA KIPAJI CHAKE KWA UWEZO WAKE,,
Knowledge is the shit,,,,

Wednesday, December 9, 2015

Sunday, November 22, 2015

EDUCATIONAL!!!




JE, NGONO KINYUME NA MAUMBILE NI SALAMA?
HAPANA, Ngono kinyume na maumbile si salama kwa sababu ina madhara mengi kiafya kama yafuatavyo;
MOJA, Njia ya haja kubwa haina vilainishi/lubrication asilia kama jinsi Uke ulivyo.
Hivyo wakati wa tendo la ngono husasani wakati wa uingizaji wa uume huwa inasababisha kuchubuka kwa tisu/ngozi laini ndani ya njia ya haja kubwa hiyo, na hivyo kupelekea michubuko ambayo bacteria, virusi na hata vimelea vingine kuweza kupenya wakati wa majeraha hayo ya michubuko na hivyo kuingia katika mfumo wa damu kupitia majeraha hayo.Hii inaweza kusababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa pamoja na VVU.

Tafiti zinaonyesha ya kuwa Ngono kwa Njia ya haja kubwa ipo katika hatari kubwa ya maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa zaidi ya asilimia 30% kuliko watu wanaotumia njia ngono kwa njia ya Uke.
Vile vile mtu anakuwa katika hatari kubwa ya kupata virusi vya human papillomavirus (HPV ) ambavyo huweza kumpelekea mtu anayejihusisha na ngono kinyume na maumbile kupata muwasho katika eneo hilo la haja kubwa na hata kupelekea kupata kansa.

PILI, Tishu ndani ya njia ya haja kubwa, haijakingwa na kulindwa kwa ngozi ngumu kama ilivyo sehemu za nje za mwili. Tishu zote za nje ya miili yetu zina ngozi ambayo ni seli zilizokufa ambazo hutusaidia kutukinga dhidi ya maabukizi ya vimelea na vile vile hutulinda na vitu tofauti katika mazingira.
Hivyo ndani ya njia ya haja kubwa hakujakingwa na ulizi huo wa asili wa seli hizo ili kuweza kuhimili, hivyo kuifanya iwe katika hatari kubwa ya kusuguliwa na hivyo kuchanika ambayo hupekea kusababisha maambukizi kuwa rahisi kutokea.

Pia ngozi ndani ya njia ya haja kubwa iko tofauti na ile ya ukeni ambapo ngozi ya ukeni huweza kuhimili ile misuguano pasipo kuweza kusababisha michumbuko kwa sababu ya vilainishi asili vinavyoatikana ndian ya uke na gozi husika.
TATU, Njia ya haya kubwa ni Maalumu kupitisha Kinyesi tu.
Kwa jinsi ambavyo njia hii imeundwa ama kutengenezwa ni maalumu kwa kuhimili na kupitisha kinyeshi tu na si vinginevyo.

Njia ya haja kubwa imezungukwa na kama misuli mfano wa ringi ama kwa kitaalamu huitwa (Anal sphincter) ambayo kazi yake ni kukaza eneo hilo kabla na baada ya kujisaidia tu.
Kipindi ambapo misuli hiyo (anal sphincter)imekazwa ama kubwa kwa kuingiziwa kitu kingine kigumu huweza kusababisha maumivu makali kwa muhusika.
Panapoendelea kuwa na mrudio wa mara kwa mara wa ufanyaji wa Ngono kwa njia hii ya haja kubwa ama kinyume na maumbile hufanya misuli hiyo ya njia ya haja kubwa kuwa dhaifu ama kulegea na isiwe na uwezo tena wakukaza kama kazi yake inavyotakiwa kufanya. Na hivyo kuwa vigumu kuweza kuzuia kinyesi kuweza kupita mpaka utapokuwa tayari kuweza kukitoa hivyo kusababisha utokaji ovyo wa kinyesi.

NNE, Njia ya haja kubwa imejaa bacteria wengi.
Njia ya haja kubwa imejaa bacteria wengi sana tofauti na Ukeni kulivyo hata kama wapenzi hawana maambukizi yeyote ya zinaa au ugonjwa wowote bacteria huwa wapo tu eneo hilo na hawa ni bacteria wa kawaida (Normal flora).
Mtu anapokuwa naingiza uume ndani ya njia ya haja kuwa anakuwa anaingiza vimelea vingine vya bacteria katika eneo hilo na wanapokutana na wale bacteria wengine waliopo katika eneo hilo husababisha madhara.

Pia pale unapohamisha uume toka katika njia ya haja kubwa na kupeleka katika Njia ya Uke badi bacteria hao utawapeleka katika eneo Uke ambapo Njia ya haja kubwa inakuwa na bacteria wengi na hivyo kupelekea maambukizi ukeni na pia maambukizi katika njia mkojo.
Ngono kwa njia ya haja kubwa inaweza kusababisha madhara mengine kwa afya ya watu wanaojihusisha na Njia hii ya ngono na wanaweza kupata madhaara kama haya yafuatayo,
Pale mdomo unapogusana na njia ya haja kubwa au kugusa uume uliotoka kwenye njia ya haja kuwa kwa mdomo kunaweza kupelekea kupata kwa wote mtu na mpenzi wake kuwa katika hatari ya kupataa magonjwa ya HEPATITIS C, HERPES/ malengelenge, kupata virusi vya human papillomavirus (HPV) na maambukizo mengine.

Hata hivyo, majeraha makubwa wakati wa ngono kwa njia ya haja kubwa mara nyingine ingawa sio kila mara hali hii kutokea inaweza kupelekea Damu kuvuja kwa ndani (hemorrhoids) baada ya tendo hilo kufanyika ambalo inaweza kusababisha au kupasuka ama kuchanika kwa misuli/nyama ndani ya njia ya haya kubwa kwa sababu ya msuguano mkali na muda mwingine hupelekea kuweza kutoboka kwa utumbo mpana(colon) hii huweza kwa ni tukio la hatari zaidi ambalo huhitaji msaada wa kitabibu haraka kwa matibabu na hata kufanyiwa upasuaji zaidi na hata kupoteza maisha kunaweza kutokea.
TANO, pia kwa wanawake wengi wanaofanya ngono kinyume na maumbile wamekuwa wakipata shida wakati wa kujifungua kwa misuli yao kushindwa kuhimili kukaza kwakati wa kusukuma mtoto na hivyo inaweza kupelekea utokaji wa kinyesi wakati wa kusukuma mtoto. jambo ambalo huleta tabu kwa wahudumu wa afya kwa kutumia muda mwigi kuwahudumia.
Njia pekee ya kuepuka kabisa hatari hizo za ngono kinyume na maumbile ni kuacha kabisa ngono kwa njia hiyo ya haja kubwa.
shiriki katika ngono kwa njia ya kawaida na ikibidi kwa kutumia kondomu ili kujilinda dhidi ya kuenea kwa maambukizi ya magonjwa ya zinaa.
Kuepuka kuingiza uume ndani ya uke na kisha mdomoni ikiwa uume ulikuwa umeingizwa katika njia ya haja kubwa.

Ikiwa umepata michubuko na kutoka damu baada ya ngono ama vidonda karibia na njia ya haja kubwa na hata katika maeneo ya uke basi onana na daktari wako haraka iwezekanavyo ili upatiwe tiba hii iakusaidi kuzuia maambukizi ya vimelea katika eneo la jeraha.
MADHARA ANAYOWEZA KUYAPATA MWANAUME ANAYEPENDA KUJIHUSISHA NA MCHEZO HUU WA NGONO NI KAMA IFUATAVYO;
KWANZA, Kunauwezekano wa Njia ya haja ndogo kuziba kiasi au kuziba kabisa kwa sababu ya vimelea kuingia na kuziba ama kuingia kwa kinyesi katika njia ya haja ndogo hivyo kukuweka katika wakati mgumu utapohitaji kujisaidia haja ndogo.
PILI,unaweza kupata magonjwa ya saratani(kansa) ya tezi tezi Prostate gland
TATU,Maambukizi ya Virusi vya ukimwi kwa sababu kuna uwezekano mkubwa sana wa kupata maabukizi tofauti na kwenye njia ya Uke hii ni kutokana na kuwa na uwezekano mkubwa wa kupata michubuko kiurahisi
NNE, Kuathirika kisaikolojia hivyo mhusika kuandamwa na msongo wa mawazo kila wakati kujutia tendo hili baya.
Nina imani ndugu msomaji wa makala hii umeweza kuona madhara mabaya sana ya tabia hii mbaya. Inawezekana umezoea mchezo huo wa kuwaingilia wenzako ama kuingiliwa kwa namna hiyo na kuona raha lakini umeziona hasara zake, amabazo kwa hakika kama wewe ni mmoja wao, unatakiwa kuacha mara moja kwa vile mwisho wake ni majuto na mateso.
Jiepushe na kuiga mambo bila kujua hasara zake, pia usimtie mwenzako majaribu kwa kumlazimisha kufanya kitendo hiki na wanaume kwa kigezo cha kuachwa kwa lengo la kuwaingilia kinyume na maumbile kwa kuwatishia kuwaacha kama watakataa.
Kipi bora kuharibiwa ama kuachwa? Jibu unalo mhusika!!
Kumbuka baada ya kuharibwa thamani yako inashuka mbele ya jamii. Kasha kupelekea kuingia katika msongo wa mawazo na mateso ya ugonjwa ama magonjwa utakayoyapata baada ya kukubali kuingiliwa kinyume na maumbile.
UKWELI MCHEZO HUU UMEWAATHIRI SANA WANAWAKE AMBAO WENGI WANAUJUTIA.
JIEPUSHE NA NGONO KINYUME NA MAUMBILE!!!!
UN

Friday, November 20, 2015

EDUCATIONAL!!!



MAAJABU 20 KUHUSU AFRIKA.!
1. Nchi ya Gambia ina chuo kikuu kimoja tu (The University of Gambia).
2. Equatorial Guinea ni nchi pekee Afrika ambayo lugha yake ya Taifa ni Kispaniola (Spanish). Hakuna nchi nyingine Afrika inayozungumza Kispaniola.
3. Afrika kusini ndiyo nchi inayotembelewa na wageni wengi zaidi kuliko nchi zote za Afrika.
4. Nigeria ndio nchi yenye matajiri wengi weusi kuliko nchi nyingine za Afrika (richest Black people).
5. Samuel Eto’o ndiye mchezaji anayelipwa ghali zaidi kuliko wachezaji wengine kutoka Afrika. Analipwa Euro 350,000 kwa wiki (sawa na shilingi milioni 980,000/=). Kwa lugha rahisi ni kwamba mshahara wa Et'oo wa wiki 7 unalingana na pesa zote alizoiba Rugemalira kupitia Escrow na kugawia kina Tibaijuka na Ngeleja.
6. Raia kutoka Nigeria anaitwa Nigerian, Raia wa Niger anaitwa Nigerien na raia wa Burkina Faso anaitwa Burkinabe.
7. Nigeria imeshinda vikombe vingi vya soka kuliko Uingereza (England).
8. Ethiopia na Liberia ni nchi pekee Afrika ambazo hazijawahi kutawaliwa. Italia ilipojaribu kuitawala Ethiopia iliishia kupigwa vibaya na ikassurender.
9. Kabila la Limba huko Zambia, mama wa mvulana ndiye anayemtafutia mwanae binti wa kuoa. Mama ndiye anayemuapproach binti, na kulipa mahari kabla hata binti hajamuona kijana mwenyewe. Kinachotakiwa ni binti kumkubali mama tu.. Ukimkubali mama means umemkubali na mwanae. So mwanae utakutana nae kwenye harusi, mambo mengine kabla ya harusi anafanya mama yake.
10. Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ndiye Rais msomi zaidi duniani. Ana degree 7 alizozisomea ktk vyuo vikuu mbalimbali, mbili kati ya hizo ni Masters.
11. Zinedine Zidane aliwahi kurudi nchi yake ya asili Algeria ili aichezee kwenye mashindano ya kimataifa. Alipofika waziri wa michezo wa Algeria, Abdelmalek Sellal akamwambia "tuna wachezaji wengi wazuri kuliko wewe na hawajapata nafasi kwenye kikosi. Labda tungeruhusiwa kucheza zaidi ya 11 uwanjani ungeweza kubatika kupata namba"
12. Robert Mugabe ndiye Rais mzee zaidi duniani. Anashikilia rekodi kwa kuwa na umri wa miaka 91 akifuatiwa na Shimon Peres, Rais wa Israeli mwenye miaka 90.
13. Shelisheli (Seychellois) ndio nchi ya kwanza duniani ambayo raia wake wameelimika kuliko nchi nyingine. Inakadiriwa kuwa asilimia 91.9% ya watu wake wana elimu ya sekondari na kuendelea. (Tanzania wenye elimu ya sekondari na kuendelea ni asilimia 13.5 kwa mujibu wa HakiElimu.)
14. Mauritius ndiyo nchi pekee Afrika inayoingiza fedha nyingi kupitia utalii wa fukwe (Beach Tourism). Mwaka 2013 iliingiza takribali shilingi trilioni 4.5 kupitia utalii wa fukwe. Tanzania tuliingiza shilingi bilioni 1.7 kupitia Utalii wa fukwe mwaka huohuo.
15. Rwanda ndiyo nchi pekee yenye usawa wa kijinsia kuliko nchi zote duniani (Bunge la Rwanda ni 50% wanaume na 50% wanawake).
16. Ethiopia ndio nchi pekee Afrika yenye viwanja vingi vya ndege vyenye hadhi ya kimataifa (International Airports). Ina viwanja vya ndege 23 vyenye hadhi ya kimataifa. (Tanzania tuna viwanja vya ndege vitatu vyenye hadhi ya kimataifa (JNIA-Dar, KIA-Moshi, na Songwe-Mbeya).
17. Uchumi wa Ethiopia unakua kwa kasi kuliko Uchumi wa China. Uchumi wa Ethiopia (GDP) unakua kwa wastani wa 18.7% kwa mwaka, China GDP inakua kwa wastani wa 11.4% kwa mwaka (according to the World bank fact sheet, 2014)
18. Rais wa Eritrea Isaias Afwerki ndiye Rais Maskini kuliko wote Afrika. Analipwa mshahara wa Dola 500 za kimarekani ($ 500) sawa na Shilingi 945,000/=. Hiki ni kiwango kidogo cha mshahara kuliko daktari wa mfunzo nchini Tanzania (Intern Doctor).
19. Angola ina watu wengi wanaoongea Kireno kuliko Ureno kwenyewe. Angola ina watu milioni 22 na wote wanaongea Kireno, lakini Ureno ambao ndio wenye lugha wana watu milioni 10.7 tu.
20. Somalia ilipata mashine yake ya kwanza ya ATM tarehe 7, October, 2014. Kabla ya hapo hakukuwa na ATM yoyote nchini Somalia.

Tuesday, November 17, 2015

EDUCATIONAL:PROCRASTINATION!!!



Kuna neno la kiingereza linaitwa PROCRASTINATION. Limenipa taabu sana kulitamka kwa muda mrefu. Linatamkwa
/prokrastineishen/. Yaani, kulitamka tu unaweza kujikuta umeahirisha😄
Ulishawahi kujikuta una mambo mengii ya kufanya. Ukajidai unajipanga ili kuanza. Wakati unajipanga unakua unachat kidogo, unaangalia tv kidogo, unapiga simu kidogo...mwisho wa siku ukajikuta hujafanya lolote kati ya mambo hayo. Ukajipa moyo "aaah, ngoja nimalizie movie nitafanya hizi kazi kesho..."
Unatamani kuanza biashara ila toka mwaka jana mpaka sasa unajisemea kimoyomoyo. "Yaani nikipata faida nanunua mzigo mkubwa zaidi...kwani Bakhresa alianzaje.."
Unatamani kusoma ila toka enzi zile unasema. "Nikianza kusoma mie breki yangu ya kwanza PhD"
Unatamani kuoa au kuolewa ila sasa miaka inapita upo tuu. "Huyu akiwa mke wangu...tutakua na watoto wazuriii...na kagari ketu wenyewe"
Huu ni ugonjwa rafiki yangu. Unaitwa PROCRASTINATION. Huu ni ugonjwa wa kuahirisha mambo kwa visingizio mbali mbali.
Napoleon Hill anasema Procrastination ni tabia mbaya, inakufanya mambo ambayo ungefanya juzi unapanga kuyafanya kesho kutwa!! Yaani jambo ambalo lilikua na kila sababu ya kufanywa kabla ya leo limewekwa lisubiri mpaka kesho kutwa.
Victor Kiam aliwahi kusema "procrastination is the assasin of opportunities". Yaani tabia hii ya kuahirisha mambo ni uuaji wa fursa. Tabia hii itakupotezea fursa nyingi.
Takwimu zinaonesha mtu mzima mmoja katika kila watu watano hua na tabia hii. Na zaidi ya nusu ya wanafunzi wote wana tabia hii.
Tabia hii hupunguza sana utendaji wako wa kazi, hukuletea stress na kuharibu afya yako, hukuletea hofu na kukufanya ujihisi mkosefu kila wakati. Hali hii hupunguza morali wa kujiamini na mwisho kukurudisha nyuma kimaendeleo.
Sababu chache kati ya ulizonazo za kuahirisha mambo ya msingi ni kama vile;
👉kutokujikubali
👉kuna wakati unajifunza na kuiga kutoka kwa watu wanaokuzunguka
👉huna uhakika kama muda ulionao unatosha kumaliza kazi hiyo
👉huamini kama una ujuzi wa kutosha
👉huoni sababu ya kufanya jambo hilo kwa kuwa faida yake ni ya muda mrefu
Kuna mtu aliwahi kusema "the best thing to get something done is to get started". Yaani kama kuna jambo lolote unataka kulimaliza basi ni lazima ulianze. Huwezi kumaliza jambo bila kulianza. Get started!!
Rafiki yangu na Rais wa City Reading Champions, Shemeji Melayeki hupenda kusema Ukiwa unaendesha gari usiku. Zile taa huonesha kipande kidogo mbele na jinsi unavyosogea ndivyo unaona mbele zaidi. Vivyo hivyo katika maisha. Kama wataka kufanikiwa katika jambo fulani basi huna budi kuanza kwa rasilimali chache na muda ulio nao. Jinsi unavyosonga mbele ndivyo utakavyokua na uwezo wa kuweka mambo mengine sawa na mwisho kufikia lengo lako.
Martin Luther King Jr. Aliwahi kusema "you do not have to see the whole staircase. Just take the first step." Yaani ukitaka kupanda ngazi ndeeefu...huhitaji kuziona ngazi zooote ili ufike juu. Anza na ile ngazi ya kwana na panda moja baada ya nyingine na mwishowe utafika kileleni.
Kama una dhamira haswa ya kufanikiwa basi sitisha na acha kabisaaa tabia yako ya kuahirisha mambo.

Saturday, November 14, 2015

EDUCATIONAL!!!


Huyu Ndie Mtu Aliejenga MUHIMBILI
HOSPITAL, ..
Anaitwa Sewa Haji Paroo, Alifika Zanzibar Akitokea Ktk Miji Ya Bhuj Na Kutch
Na Mnamo Mwaka 1852 Alifungua Duka La Bidhaa Mbalimbali Huko Zanzibar, Mnamo 1860 Akafungua Duka Lingine Kubwa Bagamoyo Na Kuweka Makazi Yake, Biashara Zake Zikawa Kubwa Na Kuwa Tajiri Mkubwa Sana, .
Alisaidia Watu Wote Bila Kujali Rangi, Dini Wala Kabila Zao, Alinunua Majengo Mengi Na Kuyafanya Maeneo Ya Watu Wasiojiweza, Alijengaja Mashule Na Hospitali Kadhaa, Ktk Mji Wa Mzizima { Leo Inaitwa Dar es Salaam}.
Alijenga Hospitali Akaiita Sewahaji
Hospitali Ikitoa Huduma Bure, Mnamo
February 1897 Sheikhe Sewa Haji Paroo
Alifariki Dunia, Ilikuwa Ni Huzuni Na Simanzi Kwa Wakazi Wa Bagamoyo Na Mzizima Kwa Kuondokewa Na Sheikhe Sewa Haji..
Aliependwa Sana, Baada Ya Kufa Kwake
Wakoloni Baadaye Wakabadilisha Jina Kutoka Sewahaji Hospital Na Kuiita Princess Magreth Hospital, Na Mnamo 1963 Iliitwa Muhimbili Hospital,
Na Mojawapo Za Wodi Inaitwa SEWA HAJI, ..
Sheikhe Sewa Haji Alale Mahali Pema Peponi....