Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Monday, June 19, 2017

STORYTELLING,BETRAYAL!!!


Since in three days its my birthday i decided to do a segment called Storytelling,A True story.
I had a friend That I concidered her as my sister,my confidant and so much more.
She knew alot about Who i am as a person and we had known eachother Since we were teenagers.
Side by side like Thelma and Louise.
Before i use to hear stories about betrayal but when you experience it its a whole different thing.
Me and this particular person we dont talk nor socialize due to betrayal and There Comes a time were you have to make a decision to test your friend and their loyalty that they claim to have,but doing so you have to be prepared for The outcome cause The truth at Times hurts but when you are ready it really dont because ultimatly it was never about you but their lack of loyalty,love,truth and honesty that they owed you.
Why live in a Lie when The truth was presented to you and God showed you Their True colours and to me that was All I needed to make The decision to Eliminate The Enemy..,

Baada ya siku tatu ni birthday yangu nikaona si vibaya nishare na nyie a personal story.
Huyu dada na mimi tulikuwa kama mtu na mdogo wake na tulijuana toka tukiwa mateenager shuleni.
Mpaka ukubwani sisi tulikuwa marafiki NO matter Huyu yuko wapi,dunka gani,anafanya nini urafiki wetu ulibaki pale pale.
Huyu dada alikuwa anajua nachofanya au nachotarajia kufanya kwani alikuwa ni mtu Wangu wa karibu.
Hakuna kitu sijamfanyia kwa lolote kwa chochote nilichoweza and lord knows I did.
Siku ikafika nikaja kujua alichonifanyia na mwanzoni nilikataa kabisa nikasema hapana haiwezekani ila mtu akija na kukuwekea ushahidi kiukweli huwezi tena kubisha so ikabidi tu nikubali shingo upande.
Baada ya mda nilijua tu kuwa lazma nifanye maamuzi and that I did.
Ukitaka kujua ukweli lazma uwe tayari kwani ukweli huwa unauma but japokuwa unauma ukweli hukupanua akili na kujua mzuri na mbaya wako.
Ukweli huja when you are ready ila ni juu yako kuukubali au kuukataa but kila mtu maishani itafika mda itambidi afanye maamuzi magumu kwenye maisha yake.
Usiogope kufanya maamuzi kwasababu ya watu kuongea watu wataongea regardless ila cha msingi ni wewe kuwa unaujua ukweli na hali halisi thats it!
Mungu hakuletei kitu tuu Bali hukuonyesha mbaya wako especially kama wewe hukuwa na nia mbaya kwake,
Maishani tutapitia mengi mno but ultimately experince na mitihani tunayopitia ndio yatakayofanya ujue how strong you are,ujasiri na pia kipi unataka au hautaki maishani mwako,Nimemaliza.com!

12 comments:

sosoano said...

well said da nuu
and pole my dia da nuu,
ndio walimwengu tulivyo, hatuna shukrani hata umlambe mwili mzima,

Unknown said...

Ni kweli kabisa na wengi hukosa ujasiri wa kukubali ukweli na kufanya maamuzi magumu.Muda mwingine tunakuwa betrayed na watu ambao tumechangia nao udugu pia. Naendelea kujifunza kutoka kwako.

Anonymous said...

Pole sana Nuru, Ila hao watu wapo kila mahali na wengine wanaletwa kwenye maisha ili kukuimarisha. Kisichokuua kitakukomaza, kikubwa ni kumshukuru Mungu kwa kuja kwake kwenye maisha yako maana amekufunza kitu ambacho labda asingekengeuka usingekijua. Kila mtu anakuja kwa sababu maalum na wakati maalum. Stay strong girl. Winnie

Irene said...

true my dear hakuna kitu kinaumiza roho kama betrayal tena kwa mtu uliyemwamini na mtu wa karibu yako sana. pole sanaaa nakuelewa mno kwa hili swala. kuna wakati unadhani hakuna maana ya urafiki

Anonymous said...

Duhhhh lisindano la kutolea damu limenichoma mfupani. yaani umegusa penyewe 'mwanangu mie'.
Yalinisibu hayo nikabaki , like, heeeee kumbe kua uyaone sio maghorofa ya Posta na mabasi ya mwendokasi, kumbe ni ya walimwengu.

Kweli dunia rangi rangile.
Unaumia but at the very end unasema, nashukuru nimelijua hili may be before sijaaanikika Zaidi na kuadhirika Zaidi.

Betrayers ni hatareeeeee na Mungu anawaona.

Mamdogo-wa-Boston

Cute Olive said...

Yani umeongea story ambayo hata mi imenipata na sikusita kuchua maamuzi magumu ila inauma kweli inaumiza sana Rafiki kua adui ni kitu kidogo sana lakini Adui kuwa rafiki hiyo haikogo. Anyway wanasema Rafiki wa kweli ni Baba na Mama yako hao hawawezi kukusaliti hata iweje.

Pole Nuru ndio kujifunza kuishi kwingi kuona mengi

Totoo said...

Well said gal. Yani hawa watu wapo sana na Mimi nishajifunza.

anonymus said...

Pole na hongera the light! Hata kwetu wapo..!mwamini

mischa said...

Inlife we have people like that around in our lives.
Pole Sana Nuru

NURU THE LIGHT said...

Thank you Winnie kwa maneno mazuri sana..
Ahsante Khadija tuko pqmojah
Yes Irene kwa mda nlisema kama huyu ndio hivi wengine je?
Mwamini o yaaaa in sam wa ukwelis vice
Thank u Mischa and Soso n Cute nimeambiwa mzigo umepata
Totoo Yes lazma tujifunze tuchague bora zaidi The next time around
Mamdogo wa Boston hahaha una captionnn...

Cute Olive said...

Yeah Nuru nilipata nashukuru sana Ubarikiwe

Bintinyota said...

katika usaliti wa marafiki, ndugu, jamaa na wandani wako; bora nikae kimya.
nimepata mafundisho mengi sana, yaani mpaka nilikuwa najiuliza lini nitaacha umamahuruma wangu?

now i know the solution is to forgive them and stay away from them.
Yaani siwapi tena nafasi ya kunijua!!
mxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx