Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Monday, January 25, 2016

WAZIRI JANUARY MAKAMBA AMSIMAMISHA KAZI!!


NI MWANASHERIA NEMC TAASISI YA SERIKALI AMBAO WALIKUWA WANASIMAMIA OPERATION BOMOA BOMOA,,

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU
KUIMARISHA UTEKELEZAJI WA
MAJUKUMU YA BARAZA LA TAIFA LA
HIFADHI NA USIMAMIZI WA MAZINGIRA-
NEMC
Katika kikao kilichoitishwa na Mhe.
January Makamba (Mb), Waziri wa Nchi
Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na
Mazingira tarehe 24 January 2016,
kuhusu kuimarisha utendaji ndani ya
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi
wa Mazingira-NEMC maamuzi yaliyofikiwa
ni kama ifuatavyo:
1. Kuhusu suala la kiwanda cha kusindika
minofu ya punda mkoani Dodoma,
imegundulika kulikuwa na ukiukwaji
mkubwa, wa makusudi na wa wazi wa
miiko ya kazi kwa watumishi wa NEMC
walioshughulika na kiwanda hicho. Hivyo,
Mhe. Makamba ameagiza watumishi wa
NEMC wafuatao wasimamishwe kazi mara
moja:
a. Dkt. Eladius Makene -Afisa Mazingira
Mwandamizi,
b. Wakili Heche Suguta Manchare -
Mwanasheria Daraja la II
c. Mhandisi Boniface Benedict Kyaruzi,
Afisa Mazingira
Hatua nyingine za kinidhamu na kisheria
zitafuatia
2. Vilevile, imebainika kwamba usimamizi
wa watumishi wa NEMC siyo makini na
thabiti na kusababisha malalamiko mengi
kuhusu utendaji wa Baraza. Hivyo,
Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Mhandisi
Bonaventura Baya apewe barua ya onyo
kalian la mwisho kwa udhaifu katika
usimamizi wa watumishi wa Baraza.
3. NEMC kama chombo muhimu nchini
kilichopewa jukumu la kusimamia
utekelezaji wa Sheria ya Hifadhi na
Usimamizi wa Mazingira inatarajiwa kazi
zake zifanyike kwa ufanisi wa kiwango
cha juu kulingana na majukumu yaliyoko
kwenye Sheria. Hivyo, kwa mapungufu
yanayojitokeza Mhe. Makamba, ndani ya
wiki moja ataunda jopo la wataalamu
wasiozidi watano ili kutathmini utendaji
wa NEMC na changamoto mbali mbali
katika usimamizi wa hifadhi ya mazingira
na kuishauri Serikali ipasavyo.
4. Ili kuimarisha ufanisi na udhibiti wa
utendaji wa NEMC, ndani ya wiki moja
litatolewa Tangazo litakalokuwa na
mambo yafuatayo: Anwani ya barua pepe
(email), Nukushi (fax), Namba ya simu,
Namba ya Whatsapp ili mtu yeyote
mwenye malalamiko au aliyewahi
kuombwa rushwa chochote na watumishi
wa NEMC ambacho ni kinyume na maadili
ya kazi yao atoe taarifa mara moja ili
uchunguzi ufanyike na hatua zichukuliwe.
5. Kutokana na mapungufu yanayojitokeza
katika utekelezaji wa Tathmini ya Athari
kwa Mazingira, ndani ya wiki moja, NEMC
ipitie upya orodha ya wataalamu na
taasisi elekezi zilizosajiliwa na kufuta
wataalamu na taasisi zote ambazo
zimekuwa zikikiuka maadili ya kazi zao
likiwemo suala la kuwasilisha taarifa zilizo
chini ya viwango, kuchelewesha kazi za
wateja wao na kutowasiliana na wateja
wao kuhusu hatua za utekelezaji wa
maombi yao.
6. Ndani ya wiki tatu uitishwe mkutano wa
dharura wa Bodi ya NEMC kujadili na
kufanya maamuzi juu ya changamoto za
utendaji katika Baraza.
IMETOLEWA NA
IDARA YA MAZINGIRA,
OFISI YA MAKAMU WA RAIS
TAREHE 24.01.2016

No comments: