Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Monday, January 25, 2016

USIKIMBILIE MUME UKAUKONDESHA MOYO MAANA WENGINE WANA STRESS SASA SIJUI ZA NINI WE SI UMEOLEWA ALIYE SINGLE AU IN A RELATIONSHIP ANAKUHUSU NINI??



NI VEMA UKAYAJUA HAYA KABLA YA KUINGIA KWENYE NDOA:
1. Sherehe ya Harusi ni ya siku moja tu, na Ndoa ni ya maisha yote.
2. Mwanamume/Mwanamke aliyezoea kuchepuka kabla ya Ndoa, ataendelea kuchepuka hata baada ya Ndoa.
3.Upole na ukimya si kiashiria cha tabia njema.
4. Ukikitaka ambacho hakijawahi milikiwa na mtu yeyote, ni lazima ufanye jambo ambalo halijawahi fanywa na mtu yeyote.
5. Mungu akitaka kukubariki hukuletea mtu, na Shetani akitaka kukuangamiza hukuletea mtu.
6. Bora uishi mwenyewe kuliko kuoa ama kuolewa na mtu hasiye sahihi.
7. Aina tatu za wanaume wakuepukwa:
a) Walevi. b) Malaya. c)Wagomvi.
8 .Kuolewa na Mchekeshaji hakutakufanya uwe na Ndoa yenye furaha.
9. Maneno matatu yanayojenga amani katika Ndoa:
a) Nakupenda. b) Samahani. c) Asante.
10. Kupiga punyeto ni kujiharibu.
11. Kuoana kabla ya kuwa marafiki ni kama anga bila jua.
12. Mafanikio ya Ndoa siku zote ni pembetatu:
Mungu mmoja - Mume mmoja - Mke mmoja.
13. Furaha ya kudumu maisha hutegemea na chaguo lako la Ndoa.
14. Usioe pesa au mali - muoe mtu.
15. Uchumba uliovunjika ni bora zaidi kuliko Ndoa isiyo na amani na furaha.
16. Usiweke kipaumbele chako kwa muonekano mzuri wa mwanamke. Hakuna mwanamke mbaya, bali anahitaji kupendezeshwa.
17. Mapenzi si upofu. Upofu ni kuoa ama kuolewa na mwanamume/mwanamke kwa kigezo tu anakidhi haja zako kingono.
18. Ukiwa rafiki mwema, utawavutia marafiki wema.
19. Asili ya mikono inayojali ni moyo unaojali.
20. Iepuke Ndoa mbaya kabla haijaanza.

No comments: