Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Wednesday, January 20, 2016

TANZANIA REVENUE AUTHORITY,MAPATO HOUSE!!!



Watu wasiojulikana wamevamia na
kuvunja ofisi ya kamishna Mkuu wa
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na
kuiba kompyuta na vifaa vingine.
Habari tulizozipata ambazo
zimethibitishwa na Polisi kanda maalumu
ya Dar es Salaam zinasema miongoni
mwa kompyuta zilizoibiwa ni ile iliyokuwa
inatumiwa na Dr. Philip Mpango
alipokaimu nafasi ya Kamishna mkuu wa
TRA kabla ya kuteuliwa kuwa Waziri wa
Fedha.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, huenda
kompyuta hiyo ikawa na taarifa muhimu
kuhusu ukwepaji wa kodi na sakata la
makontena Bandarini.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu Ya
Dar es salaam,Simon Sirro amesema
tayari jeshi hilo linawashikilia watu wanne
kwa uchunguzi zaidi.
Siro alitaja vitu vilivyoibwa katika ofisi
hiyo kuwa ni Kompyuta mbili, Televisheni
moja na King'amuzi.
Alisema wanaoshikiliwa ni walinzi wawili
kutoka kampuni ya Suma JKT ambao
walikuwa zamu usiku huo, Katibu Muhtasi
pamoja na Karani wa Ofisi hiyo.
Tangu aingie madarakani, Rais John
Magufuli amefanya mabadiliko katika
mamlaka hiyo kwa kumwondoa aliyekuwa
Kamishna Mkuu, Rished Bade na kumteua
Dk Mpango kukaimu nafasi hiyo, kabla ya
kumteua kuwa Waziri wa Fedha na nafasi
hiyo kuchukuliwa na Alphayo Kidata.
Katika kipindi hicho, baadhi ya
wafanyakazi wamewajibishwa kwa
kusimamishwa kazi kutokana na tuhuma
za ama kushindwa kusimamia vyema
ukusanyaji wa mapato au kushirikiana na
wafanyabiashara kukwepa kodi na
kulisababishia hasara Taifa.



No comments: