Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Saturday, December 12, 2015

FROM AWADH KILLO TO ALL THE MEN OUT THERE!!!

WANAUME KUWENI WAVUMULIVU KIPINDI HIKI:-

Kipindi gani hicho???

Ni kipindi ambacho mkeo ni mjamzito.

MUME KUMBUKA; wakati mkeo hana uja uzito mlistarehe na kufurahi pamoja, lkn baada ya uja uzito mke ndie anae umia na shida huzipata peke yake.

A.Mume anatakiwa azidishe mapenzi na amhurumie mkewe anapokuwa mja mzito.

B. Mletee vitu anavyokuagiza km una uwezo navyo na km huna fanya njia yyte kumtuliza na kumridhisha

C. Mpunguzie baadhi ya kazi na msaidie kazi nzito km kufua, kuchota maji nk.

D.Epuka kumlaumu, kumkasirikia , na kumpa habari mbaya km ajali, vifo vya ghafla na habar za kutisha.

E.Usimkimbie na kumuacha peke yake bila dharura yoyote.

F. Mliwaze , mpe maneno mazuri pamoja na kumbembeleza na kumdekeza.

G.Mhimize kufanya ibada ili asiache kwa ajili ya ujauzito.

H.Mwanamke anapokuwa mjamzito huwa anapata mabadiliko katika mwili wake km kunenepa sana, wengine hubadilika rangi zao na kuwa weusi, wengine hubadilika hata sura kwa kuvimba uso hivyo mume unatakiwa uvumilie.

I. Baadhi ya wanawake huwa ni wakali, watamanifu wa vitu, pia huwa hawataki hata waguswe na waume zao (tendo la ndoa), mume vumilia pia.

J. Baadhi ya wanawake huwa huwachukia waume zao, wengine hawataki hata kulala na waume zao wanaona kitanda kidogo nk , mwanamme endelea kuvumilia ni kipindi cha mpito.

Note..
Atakapojifungua ipo siku atakumbuka vituko vyake vyote na uvumilivu uliouonyesha kwa kipindi chote ataukumbuka na kujua kuwa kweli unampenda kwa shida na raha.

Subra ni muhimu ,

VUMILIA JOTO LA BEKARI ILI UWEZE KUPATA MKATE,,

Share Ujumbe huu ili uwafikie waume wote duniani.

1 comment:

Anonymous said...

What a nice msg! Nimekupenda bure mkaka, natamani wanaume wote wangeufuata huu ushauri na kuielewa hali ya mkewe kwani ni kipindi cha mpito kama ulivyosema, kubwa ni uvumilivu tu. Barikiwa sana sana.