Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Monday, November 16, 2015

SOMO LINAENDELEA!!!



Afya; Kukosa mimba kwa muda mrefu ( Zaidi ya mwaka mmoja )
Sababu zipo kuu 3
Zimhusuzo Mwanaume
Zimhusuzo Mwanamke
Zihusuzo asili "Mungu"
A Sababu zimhusuzo mwanaume
1. Kuzalisha mbegu chache… sababu zawezani kuziba kwa mirija ya kupitisha mbegu au uzalishaji mdogo au lishe duni, kuzidi kwa joto kuzunguka korodani
2. Mbegu kushindwa kuogolea kutokana kushindwa kuogelea au kukosekana kwa majimaji yenye hali ya alkali.
3. Matatizo ya uume kushindwa kuamka yaweza kuwa ni kutokana na kutumia madawa au kuumia mgongo
4. Matatizo mengine mfano matatizo ya homoni au magonjwa ya kuzaliwa/ukubwani au kutumia dawa au kutumia pombe sana
5. SABABU NYINGINE, kufanya kazi eneo lenye mionzi, kuwa na msongo wa mawazo sana, kuzidi uzito (BMI Zaidi ya 33), kuhasiwa,
B. Matatizo ya Mwanamke
6. Yai kutokukomaa. Hii yaweza kuwa ni kutokana na matatizo ya homoni, ama ya kuzaliwa au yanayotokea ukubwani
7. Mirija ya kupitisha yai kuja kwenye mji wa uzazi kuziba, hii yaweza kusababishwa na magonjwa mbalimbali ya asili na ya kuambukiza
8. Yai kurutubishwa lakini likashindwa kujipandikiza katika ukuta wa mji wa uzazi, hii yaweza kusababishwa na matatizo ya homoni, magonjwa ya asili au ya kuambukizwa
9. Umri, mayai huanza kukomaa tangu msichana akiwa na miaka yapata 14, na huacha kutengenezwa msichana akifikia miaka ya 45
10. SABABU NYINGINE… msongo wa mawazo, kutokulala vizuri, uzito mkubwa ( BMI kuzidi 33, uzito mdogo sana BMI chini ya 16.9 ) kuvuta sigara,
C Matatizo ya Mungu mwenyewe…
11. Mimba kuharibika bila sababu
12. Mimba kutokujiotesha kwenye mji wa uzazi
13. Mimba kutungwa kwenye mirija ya kusafisha yai kuja kwenyemji wa uzazi
14. Matatizo ya kijenetic katika mimba kutungwa

1 comment:

Anonymous said...

Nipo chuo, nimeona mwandishi kaandika vizuri, Usingizi ni dawa, watu wengi hawajui kukosa usingizi ni ugonjwa mbya sana, kuna watu ujisifia kwa kukesha na kujiita Mapopo, hawajui wanajimaliza.
Mwanaume; anatakiwa kulala sio chini ya masaa 6, sawa na mwanamke, athari za kutopumzika kwa mda huu tajwa, unapelekea mwanaume kupungua nguvu za kiume na mara nyingi kuchoka mapema kwenye tendo la ndoa na kuwa na msongo wa mawazo usiokuwa na chanzo, kama unampenda mpenzi wako, hakikisha unampa mda wa kutosha kupumzika.
Wanawake; kama ilivyo kwa mwanaume, mwanamke nae anatakiwa kupata mda wa kutosha wa kupumzika, sio analala saa 8 na kuamka saa 11, wale ndugu zangu wa Dar, haswa mama wa nyumbani kuamka mapema kuwaandalia watoto na baba, athari zake ni nyingi, pia mwanamke kukosa hamu ya tendo la ndoa, kuwa na msongo wa mawazo usiokuwa na sababu maalum, kuwa na hasira kila mara hata kwenye vitu vidogo, hii inaweza kumpelekea hasishike ujauzito au mimba kutoka, ivyo wewe kama ni mwanamke unaejitambua panga ratiba yako vyema na hakikisha unalala vizuri.