Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Friday, November 20, 2015

BUNGENI DODOMA!!!

Unazungumziaje kitendo cha wabunge wa UKAWA kupiga kelele wakitaja jina la Maalim Seif wakati viongozi wa Zanzibar na Rais Magufuli wakiingia Bungeni leo na kisha kutoka nje baada ya kuamriwa na Spika,,

Aliyeingia hivi sasa Bungeni katika uzinduizi wa Bunge ni Rais wa Zanzibar Dkt Ali Mohamed Shein,kelele nyingi zinasikika kutoka kwa wabunge wa UKAWA wakipinga kutomtambua huku wakilitaja jina la Maalim Seif

Kelele za wabunge zinaimba "Maalif Seif, Maalim Seif, Maalim Seif, Maalim Seifu..." Lakini taratibu zinaendelea

Spika wa Bunge Job Ndugai amewaamuru wabunge wanaopiga kelele watoke nje. Askari wameingia na kuwaamuru wabunge watoke nje, wabunge wote waliokuwa wakipiga kelele wametoka nje,,

2 comments:

Unknown said...

Ni uthibitisho tosha kuwa mamlaka zinazotunga sheria wao wenyewe wanashindwa kuziheshimu na kuzisimamia sheria walizotunga. Sheria ya Uchaguzi ile ya Zanzibar na hata ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania inasema Kutakuwa na Tume Huru ya Uchaguzi. Maamuzi ya tume hayataingiliwa na utashi wa mtu yeyote au chama chochote. Tume ya Zanzibar imefuta uchaguzi wa Zanzibar kwa sababu kadhaa walizozitowa kwamba zimekiukwa, sasa kwanini hawataki kuheshimu hilo.
Sheria ya Uchaguzi inakataza mgombea kujitangazia ushindi yeye mwenyewe huyo Maalim Seif nini alifanya nadhani kila mmoja aliona. Baya zaidi kitendo hicho alichokifanya Maalim Seif mbali ya kuzua sintofahamu lakini hakuna UKAWA yeyote aliyelaani ukiukaji huo wa sheria. Kwahiyo ndio maana ninasema kitendo walichokifanya ni uthibitisho tosha wa mamlaka za kutunga sheria au tuseme baadhi ya watunga sheria wanashindwa kuheshimu sheria wanazotunga wao wenyewe............!!!
Kwa ufupi ni kitendo cha kujiabisha wao wenyewe............!! Kama utasoma na kuielewa vizuri katiba ya Zanzibar utaona ukomo wa raisi wa Zanzibar unaishia lini....! Maalim Seif ametangazwa kuwa mshindi au amejitangaza? Maalim Seif Ameapishwa kuwa Rais wa Zanzibar?

Unknown said...

UKAWA WAMESHINDWA KUJITAMBUA....!!! MBAYA ZAIDI NI ASUBUHI MMNOOOO