Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Friday, May 15, 2015

LIKE I SAID KWA KUKUZA TUU!!!



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
BASATA Arts Centre
Ilala Sharif
Shamba
P.O. Box. 4779, Dar es Salaam
E-mail:basata06@yahoo.com
Tel. 2863748/2860485
Fax: 0255- (022) – 286 0486 BASATA YALAANI
TABIA CHAFU NA ISIYO NA MAADILI
ILIYOONESHWA NA MSANII SHILOLE KWENYE
ONESHO LAKE NCHINI UBELIGIJI
Staa wa Bongo Fleva, Zuwena Mohamed ‘Shilole’
akiimba kwa hisia nchini Ubelgiji.
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ambalo ni
msimamizi wa sekta ya Sanaa na burudani
nchini limeona picha chafu na zisizo na maadili
za Msanii Zuwena Mohamed maarufu kama
Shilole alipokuwa akifanya onesho lake nchini
Ubeligiji hivi karibuni.
Katika picha hizo ambazo zimelaaniwa na
watanzania wengi nchini kupitia njia mbalimbali
ikiwemo mitandao ya kijamii, Shilole anaonekana
akiwa Jukwaani huku viungo vyake vya sehemu
za siri vikiwa hadharani na zaidi akionesha tabia
ambazo kwa kiasi kikubwa zimefedhehesha na
kuidhalilisha sekta ya Sanaa na Taifa kwa
ujumla.
Aidha, BASATA limepokea malalamiko kwa njia
ya simu na mawasiliano ya internet kutoka kwa
watanzania waishio ughaibuni wakilaani tukio la
Msanii huyo. Katika mawasiliano yao wameeleza
kwamba wamefedheheshwa na kudhalilika na
tabia hiyo chafu iliyooneshwa na msanii huyu.
Ikumbukwe kwamba, Shilole ni msanii
aliyesajiliwa na Baraza la Sanaa la Taifa, hivyo
anapokwenda nje ya nchi kabla hajapata visa
anapewa barua ya utambulisho kama msanii wa
Tanzania, hivyo anapokuwa nje ya nchi
anatambuliwa kama msanii Mtanzania,
anapofanya kinyume na misingi ya kazi ya
Sanaa, anajifedhehesha yeye mwenyewe, kazi
ya Sanaa na nchi yetu pia.
Aidha, ikumbukwe kwamba BASATA limeshapata
kumwita na kumuonya msanii huyu kutokana na
tabia yake ya kutokujiheshimu pale awapo
jukwaani na yeye aliahidi kubadilika na
kuachana na tabia hiyo chafu. Kwa hiyo
kuendelea kwake kufanya matukio hayo na kwa
sasa katika ardhi ya nchi nyingine ni uthibitisho
kwamba hajabadilika na kwa maana hiyo
ameendelea kuidhalilisha Sanaa na wasanii wa
kitanzania wenye kujitambua na kuiheshimu
Sanaa kama kazi nyingine.
BASATA linapenda kueleza kwamba;
Litamuita kwa mara nyingine tena kumtaka
ajieleze kwa nini alifanya onesho hilo la
kujidhalilisha na kudhalilisha hadhi ya
mwanamke, msanii na Sanaa kwa ujumla
Kama maelezo yake hayataridhisha hatua kali za
kinidhamu zitachukuliwa dhidi yake maana
tayari ameshadhihirisha kwamba akifanyacho si
Sanaa na hakina uhusiano na kazi ya Sanaa
ambayo ina heshima yake na inahitaji ubunifu,
weledi na kujitambua
BASATA linawakumbusha wasanii wote nchini
kuwa Sanaa ni kazi kama kazi zingine lakini siku
za hivi karibuni wasanii wengi wamekuwa
wakikiuka suala zima la maadili kwa kutengeneza
kazi chafu zisizofaa mbele ya jamii ya
watanzania wanaoipenda na kuiheshimu kazi ya
Sanaa yenye staha. Tuungane kwa pamoja
kukemea kazi chafu zinazozalishwa na wasanii
wasiojitambua kwani suala la maadili ni suala
mtambuka na linaanzia katika ngazi ya familia.
Aidha, BASATA linawataka Wasanii wote nchini
kufuata sheria, kanuni na taratibu mara
wanapopata mialiko ya kikazi kwenda nje ya
nchi. Linawakumbusha kwamba haiwezekani
msanii kutumia picha chafu na mavazi dhalili na
kuonyesha utupu katika kuvuta mashabiki.
Sanaa ni kazi, tuipende na kuithamini
Godfrey Mngereza,,

BASATA linapenda kueleza kwamba;
  1. Litamuita kwa mara nyingine tena kumtaka ajieleze kwa nini alifanya onesho hilo la kujidhalilisha na kudhalilisha hadhi ya mwanamke, msanii na Sanaa kwa ujumla
  2. Kama maelezo yake hayataridhisha hatua kali za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yake maana tayari ameshadhihirisha kwamba akifanyacho si Sanaa na hakina uhusiano na kazi ya Sanaa ambayo ina heshima yake na inahitaji ubunifu, weledi na kujitambua
BASATA linawakumbusha wasanii wote nchini kuwa Sanaa ni kazi kama kazi zingine lakini siku za hivi karibuni wasanii wengi wamekuwa wakikiuka suala zima la maadili kwa kutengeneza kazi chafu zisizofaa mbele ya jamii ya watanzania wanaoipenda na kuiheshimu kazi ya Sanaa yenye staha. Tuungane kwa pamoja kukemea kazi chafu zinazozalishwa na wasanii wasiojitambua kwani suala la maadili ni suala mtambuka na linaanzia katika ngazi ya familia.
Aidha, BASATA linawataka Wasanii wote nchini kufuata sheria, kanuni na taratibu mara wanapopata mialiko ya kikazi kwenda nje ya nchi. Linawakumbusha kwamba haiwezekani msanii kutumia picha chafu na mavazi dhalili na kuonyesha utupu katika kuvuta mashabiki.

BADALA MCONCETRATE NA HAKI ZA WASANII YOU WORRY ABOUT THIS,,HAHAHAH WONDERS SHALL NEVER SEE WOOO!!!
BADALA MKEMEE PIRACY NA HAKI ZA KAZI ZA WASANII ILI WASIFE MASKINI YOU WORRY ABOUT THIS,,

1 comment:

Anonymous said...

Upuuzi mtupu. Shilole ana maamuzi yake binafsi ya kujiexpress anavyopenda kama binadamu huru. Mimi kama mwanamke wala hajanidhalilisha wala nini. Kama kujidhalilisha ni yeye mwenyewe kwa maamuzi yake. Acheni unafiki watanzania kujifanya watu wa maadili wakati hakuna. Kungekuwa na maadili isingekuwa okay kwa wanaume wa tanzania Kuwa na nyumba ndogo openly na watoto wa nje za ndoa bila kujificha. Shame.