Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Tuesday, April 1, 2014

FACEBOOK STATUS FROM ZA QUISHA!!!





"Nkimaliza zangu Chuo ntaaplai zangu kazi Voda, ntalipwa milioni 3.5/mwezi, ntajibana zangu kila mwezi natumia laki5 tu, izo 3m naifaZi benki, baada ya miezi mi3 nanunua gari la 9m/=, nkishakua na gari basi 3m ya mwezi unaofatia napanga nyumba ya laki mbili na amsini kwa mwezi, 3m inayofatia nanunua fenicha, kwanza adi apo ntakuwa nshatimiza miezi 6 kazini, adi apo naruhusiwa kukopa, nakopa zangu 10m/= afu natafuta kiwanja cha 6m tu, si ntakuwa nakatwa 1m/= za mkopo kila mwezi, izo 4m nafungua kabishara, bado ntakuwa nabakia na 2m/= /mwezi baada ya makato ya mkopo, izo 2m zinatosha kila mwezi kupandisha tofali, Mungu jaalia kabla Jakaya ajatoka madaLakani, nna mjengo, gari na kijibiashara changu pale Mwenge.
.
Mliosoma vyuo naamini mmewahi kuwa na muono huo mkiwa chuoni, huu muono unapangika fresh sana, huitaji hata Kalkyuleta, hii kwa kizungu inaitwa "Theory", wahisani wetu Watu wa Marekani wanaitaga "PLAN A". Maliza chuo sasa uje mtaani, utakutana na kitu kwa kizungu inaitwa "Implimentesheni", ndo neno "PLAN B" linapokujaga, plan B kuielezea ni ngumu labda nitunge sentensi fupi huyo kijana apo juu atayoituma akitoka zake Job, of kozi mwezi wake wa 10 job: "Mwana shwari, leo nmetoka mapema mwana ila sina hata ela ya Bajaj, mwana unawezakuwa na efamsini ya karibu Mkuu nmalizie ngwe, ntakurudishia mwisho wa mwezi mshahara ukitoka, sijasteblaizi bado mwana!"

2 comments:

Anonymous said...

MHHHHHHHHHHH ukipata mshahara wa hivyo mbna unashukuru sna hyu MUNGU n rahisi sana kusema lkn duuuuuuuuh hpo lzma akiingia kitaa aje n plan b...hahahahahaha

Anonymous said...

hahahahaa kwa bongo hapa unahitaji kuwa na plan c ukimaliza chuo.maisha ni noma kitaani.