Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Wednesday, April 11, 2012

ELIZABETH MICHAEL!!


#LULU KIZIMBANI LEO

Muigizaji wa Filamu nchini anaehusishwa na kifo cha Muigizaji Mwenzie,Marehemu Steven Kanumba,Bi Elizabeth Michael a.k.a Lulu amepandishwa kizimbani mapema leo asubuhi kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam kwa kusomewa mashtaka yake kuhusiana na kuhusika kwa kifo cha Muigizaji huyo nguli hapa nchini.

Elizabeth Michael amesomewa mashtaka hayo mbele ya hakimu Agustino Mmbando na wakili Elizabeth Kaganda ya mauaji ya Muigizaji wa Filamu nchini,Marehemu Steven Kanumba yaliyotokea huko sinza vatcan jijini Dar es Salaam april 7 mwaka huu.

Elizabeth Hakutakiwa kujibu chochote Mahakamani hapo kwani mahakama hii haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji. Kesi hiyo imeahirishwa na kupangwa kusikilizwa tena april 23 mwaka huu. Muigizaji huyo aliletwa mahakamani hapo kwa mwendo wa kasi kama mshale na kwa ulinzi mkali na pia ndivyo alivyoondolewa Mahakamani hapo Kwa gari ndogo nyeupe aina ya suzuki grand vitara yenye nambari za usajiri T 848 BNV huku kwenye kioo nambari zake zikisomeka PT 2565.

BBC SWAHILI HAD THIS TO SAY;

Amefikishwa mahakamani ikiwa ni siku nne, tangu alipokamatwa mara baada ya kifo cha msanii huyo ambaye inaaminika kuwa walikuwa na uhusiano wa Kimapenzi.
Taarifa zinazohusiana
Afrika, Tanzania
Mbele ya Hakimu mfawidhi wa Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam,Bi Augustina Mbando,Elizabeth Michael Kimemeta ajulikanaye kama Lulu kwa jina la Usanii,aliwasili mahakamani hapo akiwa chini ya Ulinzi mkali wa askari Polisi waliokuwa wamevaa kiraia na wengine wakiwa wamejihami kwa silaha.
Mara baada ya Kufikishwa mahakamani,upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa serikali Bi Elizabeth Kaganda ulimsomea shtaka moja ambalo ni la mauaji, kosa ambalo ni kinyume cha sheria ya kanuni ya adhabu kifungu cha 196.

Wakili huyo wa serikali Bi Elizabeth Kaganda,alidai mbele ya mahakama kuwa mnamo tarehe 07 mwezi April mwaka 2012,katika eneo la Sinza Vatican,msanii Elizabeth alimuua msanii Steven Kanumba.

Akiwa amevalia gauni kubwa lijulikanalo kama dera lenye rangi ya Njano mtandio wa rangi ya waridi na kandambili nyekundu mshtakiwa alionekana kutokuwa na wasi wasi pamoja uzito wa tuhuma za mauaji anayokabiliwa nayo huku akijibu maswali kadhaa kuhusu wasifu wake.
Msanii huyo alikanusha kuwa na umri wa miaka 18 baada ya kuulizwa ,ambapo yeye amesisitiza kuwa ana umri wa miaka 17, hii ikiwa ni tofauti na habari ambazo zimekuwa zikiripotiwa kuhusu umri wa msanii huyo ambaye sasa anatambulika kama mshtakiwa.
Kesi hii ya mauaji inatajwa kwa mara ya kwanza na mshtakiwa hakutakiwa kukiri wala kukana mashtaka.
Upande wa mashtaka umeieleza mahakama kuwa kesi bado iko kwenye upelelezi ambapo inatarajiwa kutajwa tena April 23 mwaka huu.
Mshtakiwa amepelekwa rumande hadi siku hiyo wakati kesi hii itakapotajwa tena.
Kwa upande mwingine tukio la kufikishwa mahakamani kwa mtuhumiwa huyo kumefanywa kwa usiri mkubwa na kufanya waandishi wa habari wengi wameshindwa kufuatilia kwa karibu tukio lenyewe.
Kufikishwa mahakamani kwa msanii huyo na kusomewa shtaka la mauaji ya Kanumba kumetokea siku moja baada na Marehemu Steven Kanumba kuzikwa katika makaburi ya Kinondoni.
Mazishi yake yalichukua sura ya kitaifa kutokana na umaarufu aliojijengea msani huyo katika jamii ya watanzania na hata nchi za nje.

8 comments:

Jestina George said...
This comment has been removed by a blog administrator.
Anonymous said...

Nuru hii ni picha ya leo? pole lulu wewe nimwanamke mwenzangu,na vile vile pole mama kanumba na pole mama lulu kesi ni ngumu.

NURU THE LIGHT said...

ukisoma maelezo wameandika leo alikuwa amevaa dira na mtandio so sio ya leo,,,hii kesi sio rahisi kabisa we just have to wait n see,,,

Anonymous said...

ok sikusoma maelezo kabisa Nuru maana nilijua ni yale yale maelezo ya kwa kaka michuzi,nilikuwa naulizia picha sababu kavaa nguo nyeusi na hao wanajeshi huko nyuma,sorry niko nje ya nchi.ni swali tu,. stay blessed.

NURU THE LIGHT said...

hii ni kesi yake ya zamani na haikuwa kubwa kihivyo ndio hii picha ilipigwa,,hamna shida mdau nilikuelewa vizuri tuu,,ahsante

Anonymous said...

LULU IS GUILT UNTIL PROVEN INNOCENT, AND SHE HER SELF IN MIKASI SHE CONFESSED THAT SHE IS 18 SO SHE SHOULD JUST ASK FOR FORGIVENESS AND HER SENTENCE TO BE MINIMAL. HAKI LAZIMA ITENDEKE...POLE SANA LAKINI ILA ULIONYWA NA JAMII NZIMA NA HUKUTAKA KUTULIA

Anonymous said...

haya ni maoni tu hapa tayari ameshitakiwa kwa kosa la mauaji lkn kesi bado inaendelea na uchunguzi, kwa ufahamu wangu ni kwamba ni mpaka pale DDP atakaporidhishwa na vielelezo ndipo mshtakiwa atakuwa na kesi ya kujibu sasa hapa sijui imekaaje tungoje tusubiri. lkn hapa ni lazima kutakuwa na ukiukwaji wa sheria kwanza kabisa nyumba ya marehemu yalipofanyika hayo mauaji ilitakiwa ifungwe kabisa. watu wa mwisho waliokuwa kwenye tukio akiwamo mdogo wa marehemu wote walitakiwa washikiliwe kwa uchunguzi. taratibu nyingi zimekikwa ikiwa ni pamoja na kumuondoa marehemu eneo la tukio kabla ya uchunguzi. hata kama alisukumwa ushahidi utakuwa umeshapotea kwa kuwa tayari kutakuwa na fingerprints za watu wengine waliombeba na kumvalisha nguo kama inavyodaiwa. mazingira yote ya kesi yamegubikwa utata mtupu. mungu mwenyewe ndio anajua.

NURU THE LIGHT said...

LULU IS 17 AND NOT 18...,KUNA WATU WENGI HUWA WANADANGANYA KWENYE INTERVIEWS SHE IS NOT THE FIRST NA HATOKUWA WA MWISHO..,TUSUBIRI TU KESI ITAVYOENDELEA..,