Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Monday, November 2, 2015

DEE!!


JAY Z!!!


THEN AND NOW!!




I HEART!!!






MWISHO WA KUMTAKIA MTU MABAYA NI MBAYA!!!!



FROM A FATHER TO HIS SON!!!



1. Mwanangu, mwanamke anaweza kuwa mkeo, mwingine anaweza kuwa mama wa watoto wako, lakini ukipata mwanamke ambae atakuwa kama mama kwako, mama kwa wanao na mama kwa familia, tafadhali mwanangu usimuache huyo!
2. Mwanangu, usimfanye mwanamke wako kuwa ndio wa kupika na kufanya kazi zote za jikoni peke yake, tabia hiyo sio nzuri Kwani hata nyakati zetu, mashamba yetu yalijulikana kwa majina yetu wanaume lakini tulifanya kazi pamoja!
3. Mwanangu, nikikwambia wewe ni kichwa cha familia, simaanishi kutuna kwa pochi lako, usiangalie kabisa pochi yako, angalia kama utaona tabasamu usoni kwa mke wako. Pesa sio kila kitu katika ndoa na haileti ukuu wa familia!
4. Mwanangu, ukitaka kuwa na maisha marefu na ukapunguza misongo ya mawazo, ongea na mkeo pangeni bajeti ya mahitaji yenu, kisha mwache mkeo awe na jukumu la kuratibu mahitaji ya kila siku ya familia kwa kumkabidhi fungu husika hata kama limetokana na michango yenu wawili. wanawake wanajua sana kupanga bajeti na hii haitakuwa rahisi kwa yeye kutumia hela hovyo wakati akijua kuwa nyumbani kuna mahitaji ya msingi, lakini hela zikiwa mikono mwako ataendelea kuomba hata kama utakuwa umeishiwa!
5. Mwanangu, Usithubutu kumpiga mkeo, maumivu ya kipigo hukaa ndani ya moyo wake kwa muda mrefu sana na huacha kidonda ambacho hukawia sana kupona. Ni hatari sana kuishi na mwanamke mwenye majeraha moyoni!
6. Mwanangu, sasa unaamua kuoa,kama bado utaendelea kuishi maisha kama ya ubachela na mke wako, sio muda mrefu utakuwa bachela tena. ukioa Badilika anza kuishi maisha ya mke na mume!
7. Mwanangu, zamani,tulikuwa na wake wengi na watoto wengi kwa sababu tulikuwa na mashamba makubwa na mavuno yalikuwa makubwa, lakini kwa sasa maisha yamebadilika, kwa hiyo mkumbatie mwanamke wako peke yake kwani hakuna ardhi tena na mahitaji ya watoto ni makubwa sana. Angalia ukubwa wa familia yako!
8. Mwanangu, chini ya mwembe ambao nilikuwa nikikutana na mama yako inaweza kuwa ni hoteli kubwa kwa nyakati zenu,lakini kumbuka, kitu pekee tulichoweza kufanya chini ya mwembe ilikuwa ni kukumbatiana pekee.nakushauri ukikutana na marafiki wa kike kikubwa unachoweza kufanya nao ni kupeana mikono na ikizidi ni kukumbatiana hadharani sio vinginevyo!
9. Mwanangu, usibadilike mara utakapoanza kupata mafanikio Zaidi, kuliko kuwahudumia hao viruka njia wa mtaani ambao hawajui mmetoka wapi na mkeo, nakushauri utumie na kufurahia mafanikio yako na mkeo ambae aliweza kusimama imara wakati wote wa mapito yenu magumu.
10. Mwanangu, kumbuka unapoanza kusema au kuona mke wako kabadilika, ujue kuwa kuna kitu ambacho ulikuwa ukikifanya umeacha kukifanya. Jitathmini na anza kufanya au kutimiza wajibu wako.
11. Mwanangu, usijaribu kumfananisha au kumlinganisha mke wako na mwanamke mwingine wa nje, kwani hata yeye anakuvumilia sana na hajakufafanisha na mwanaume mwingine yoyote huko nje na ndio maana aliamua kuwa na wewe.
12. Mwanangu, sasa hivi kuna hiki kitu kinaitwa haki za wanawake, sawa,kama mwanamke anasema ana haki sawa na wewe katika nyumba, basi gawanya mahitaji yote ya ndani kwenu katika sehemu mbili zilizo sawa,halafu timiza nusu yako na mwambie atimize nusu iliyobaki.
13. Mwanangu, nilimuoa mama yako akiwa bado kigoli (bikra) na nilikuwa naenda sana kwao kabla sijamuoa, lakini kutomkuta mkeo bikra kusikufanye umlaumu kuwa alikuwa muhuni, kumbuka wanawake wa enzi zetu na wasasa ni tofauti, ulimchagua mwenyewe na ukigoli wake hukuujua kabisa. Usiingize mambo ya kabla ya ndoa kwenye ndoa yenu.
14. Mwanangu, sikuwapeleka dada zako shule kwa kuwa nilikuwa mjinga kama wazee wengi wa hapa kijiji wasemavyo, tafadhari usifanye ujinga huu, kwani kiwango cha mafanikio ya wanawake sasa kimefanya wanaume waonekane ni watu wa kawaida sana na sio muhimu kama enzi zetu. Ukijaliwa watoto wape elimu.
15. Mwanangu, zamani enzi za ujana wetu, wanawake walikuwa na urembo wa asili, ingawa siwezi kukudanganya, wengine waliongeza urembo kwa kujichora hina na hata kutoboa pua na masikio lakini usisahau hawakuonyesha maumbile yao nyeti hadharani kama sasa. Hakikisha mkeo analijua hili!
16. Mwanangu, mama yako na mimi hatuna hisa katika kila kitu kinachoendelea kwenye maisha yenu, jaribuni kutatua changamoto zenu wenyewe bila kila mara kuja kwetu kuomba usuluhishi. Ndoa ni pamoja na ukomavu wa kutatua changamoto zenu bila kuziuza kama gazeti kwa kila mtu.
17. Mwanangu,nilimnunulia mama yako kifaa cha kupikia vitumbua ili aanzishe mradi wa kuuza vitumbua, pia nilimsaidia kununua cherehani yake ya kwanza, tafadhari msaidie mke wako kutimiza ndoto zake kulingana na uwezo wako kama ambavyo unahangaika kutimiza ndoto zako.
18. Mwanangu, usiache kutusaidia mimi na mama yako, utu uzima una changamoto nyingi sana na Mungu akikujalia utaziona muda ukifika. Pamoja na kutimiza majukumu yako kama baba wa familia kumbuka pia bado tunaishi na wewe ni mtoto wetu.
19. Mwanangu, kila upatapo muda wa kusali, Sali na familia yako, kuna kesho ambayo huijui, ongea na MUNGU wako ambae anajua kila kitu kila siku!
20.NAKUTAKIA MAISHA MEMA YA NDOA MWANANGU….NAKUPENDA!


THE EARCUFF!!!






Sunday, November 1, 2015

A HALLOWEEN WELL SPENT WITH LA FAMILIA,KÄRLEK!!!










 THE TURBAN;GIFT FROM MY COUSIN
BOOTS;ECCO
DRESS;H&M
LIPSTICK;LANCOME COFFEE DATE



SINCE I HAVE BEEN WORKING SO MUCH I HAVENT SPENT ALOT OF TIME WITH LA FAMILIA SO THE HALLOWEEN WEEKEND FELT JUST PERFECT,,
COOKED SOME FOOD ALL OF THIS FOOD I MADE WAS A SPECIAL REQUEST CAUSE HALLOWEEN IF YOU WANT TO GO ALL OUT ITS EVEN MORE FUN BUT HEY WE KEPT IT OUR WAY,,
THE KIDS WENT TRICK A TRIIII AROUND THE NEIGHBOURHOOD AND AFTER WE STARTED THE CELEBRATION,,
I GUESS THE PICTURES SPEAKS IT OWN LANGUAGE,,
UNTIL NEXT YEAR HAPPY HALLOWEEN FOLKS!!!





THAT!S ALL FOLKS,,UNTIL NEXT YEAR!!!

WIZKID IN TANZANIA!!!



IMAGES;WWW.BONGO5.COM

KUNA AMBAO WALISHANIOMBA MSAMAHA NA KUNA AMBAO BADO NASUBIRI WANIOMBE MSAMAHA,THE CHOICE IS YOURS!!



Dada mmoja alikuwa airport akisubiri connetion ya ndege yake, wakatangaziwa ndege itachelewa saa mbili zaidi.
Akaamua kununua gazeti na box Dogo la biscuits, akatafuta sehemu akakaa kusoma gazeti kusubiri muda ufike wa kuingia kwenye ndege, alipokaa pembeni yake kulikuwa na kaka nae anasoma gazeti akisubiri ndege. Dada alishangaa alipokuwa akitoa biscuit kwenye box aliloliweka pembeni yule kaka nae anachukua moja anakula, akamwangalia kwa hasira, kaka akawa anatabasamu.
Dada akakasirika akataka kumtolea maneno machafu akajizuia. Ukawa mchezo kila dada akichomoa biscuit moja yule kaka nae anachukua moja. Ikaendelea hadi ikabakia biscuit moja.
Yule kaka akawahi kuichukua akaimega nusu akampa yule dada, ...dada kwa ghadhabu akanyanyuka akamtukana sana yule kaka na maneno ya kumdhalilisha kwanini anavamia vitu vya watu asinunue vyake!! Kaka alikaa kimya bila kumjibu yule dada.
Mara wakatangaziwa muda wa kuingia kwenye ndege umefika. yule dada akaingia akimuacha kaka nae akisubiri ndege yake.
Alipokaa kwenye siti yake akafungua mkoba aweke simu yake, mara alishtuka kuona box lake la biscuits zima wala halijafunguliwa, kumbe alikuwa anakula biscuits za yule kaka. Akajutia sana akatokwa na machoz jinsi alivyomdhalilisha yule kaka, na muda wa kurudi kuomba msamaha haupo tena kwani milango ya ndege ilishafungwa na kuanza kuondoka.
"Muda wa kuomba msamaha kwa uliyemkosea upo usisubiri milango ifungwe"...
Kiburi, wivu, husuda ni sifa za Ibilisi.
Nawatakia jumapili njema nyooote! Kama umemkosea mtu, umemsingizia ili aonekane mbaya au ukimsema huku ukijua sio kweli unachosema au ukimharibia mtu maisha, wahi kumuomba msamaha kabla milango haijafungwa🙏🏽⏰⌚🕗
UKIIPENDA SHARE TAFADHALI KAMA NILIVYOFANYA MIMI!