Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka
Showing posts with label Shamba life. Show all posts
Showing posts with label Shamba life. Show all posts

Thursday, April 6, 2017

WHEN YOU FIND YOUR DREAM STANDING RIGHT INFRONT OF YOU!!!



























Tanzania ni nchi nzuri na yenye ardhi na maandar nzuri.
Nadhan kwenye swala la kununua shamba au kiwanja au viwanja ni kitu nimeshawakumbushia sana na kuwahamasisha vya kutosha kwahiyo sina haja ya kufanya hivyo tena kwani mnaona na kushuhudia through mimi na wengine wengi.
Bakhresa ana ardhi au kanunua ardhi mashallah ila yeye ana uwezo mkubwa but non the less Bakhresa ameanza chini sana mpaka kufikia hapo alipo na bado hajaridhika Bali bado ana invest nchini na kuteka soko by soko.
Nilisema nitaanza na kimoja which i did miaka kadhaa nyuma Bali nikasema kwanini ni stop here kwani ardhi huwa haishuki thamani Bali hupanda.
Nimeanza KUGUNDUA kuwa kuna watu wanaingia humu ila hawasomi au hawaelewi ninachoandika but that is not my problem kwani kila kitu ni perception nikimaanisha sio kila mtu ataelewa maana wengine wana yao kichwani na moyoni.
Sio kila aloenda shule means kaelimika kwani wengine walikuwa hata madftari hawabebi.
INLIFE tutakutana na watu wazuri na wa ajabu, tutakutana na wataotushika mkono na wale watakaotaka uangamie.
Wengine walikuwa wanasubiri udhalilike ila kila kukicha wanaona unazidi kuwa na maarifa na kuwa na maendeleo sasa unategemea watafurahia?
Nilimsaidia mtu akaja kunipa ahsante a year after wakati nilishasahau sasa kama hakuona umuhimu then why imekuwa important all of a sudden so you see hivi ni vitu tunapitia tu na KUTUFUNZA kwa ajili ya kesho.
Kuna watu leo hii wanaandika maneno mazuri mitandaoni na mnayasoma na kuwaadmire ila hao hao watu damu yao hawajui wamekula nini saa hii.
Kuna mtu hajampa mama yake buku tu wakati anaspend laki 5 kwa watu baki so you see sisi wanadamu kila mtu anapriority zake so usidhani hata ukimuonyesha maarifa atayapokea kwani kwa sasa hayuko tayari.
Kama Dullayo anavyosemaga Nuru haters motivates us mimi huwa namjibu hapana mimi wanaonimotivate ni waliofanikiwa na wale wanaoamka kila siku kutafuta Chao kwa jasho lao kwaajili ya wao na familia zao,Nimemaliza.com!!

Tuesday, April 4, 2017

SHAMBA HUNTING#FARM HUNTING#SHAMBALIFE!!!





 When my eyes saw him I instantly fell inlove..,












 Chocolate..,


 Bye Kids I gotta go,.,



If you ever going to rent or purchase anything in the world make sure to do your homework and your research prior to and make sure that the pappers are in order and most importantly the property is indeed in full.It is important to make sure that you protect yourself incase of anything but make sure that  the law is in your favor at all times since we got som dishonest people so it is important to take your time,make sure everything is in order and then make the purchase.
Don't be scared of asking the right questions and dare to challenge the seller with thee right questions so that you get all the answers to your questions which will be helpful to you.

Ukiwa unataka kununua kitu au kukodisha kitu Sehemu yoyote ila dunIani usiwe muoga kumchallenge mtu unayedeal nae kwani kwenye maswali yako na changamoto maswali unayompa ndio utapata jua mengi na offcoz kuna matapeli ambao wanapractise jibu la swali lolote lile bali na wewe pia unatakiwa uwe mjanja na kingine do your homework usiende tu jicho moja fanya research na usiwe na papara na ikiwezekana nenda kila idara inayotakiwa kuhakikisha je unachouziwa ni halali au kiko kwenye utdata.
Nimegundua Tanzania ni kubwa sana nourri.
Uzuri wa Tanzania unaweza kukaa popote PALE as long as una usafiri yaani swali la usafiri likishughulikiwa nawaambieni sehemu kama Sinza,Kariakoo sijui Kinondoni mtapaona hapafai kwa ubanano IT IS TRULY AMAZING kuwa nayaona haya leo japokuwa upande mwingine naona kama nimechelewa na hapo sijatembea sana mikoani nadhan nitachanganyikiwa kwa uzuri wa nchi yetu ila unaambiwa in life kila kitu kinaendana na TIMING.

Wednesday, March 22, 2017

RESPECT MY HUSTLE CAUSE IT TAKES WORK,DEDICATION,DISCIPLINE AND WILL POWER TO TURN THE DREAM INTO REALITY!!!










 MASHALLAH YAMEKUWA VIZURI SANA.,

 Asante mungu am happy to see progress but also my hustle,,









 Mtoto nilokuwa nimembeba ni wa huyu kaka mtuwangu wa nguvu..,Mungu azidi kukuweka!
 Akinieleza mengi na kunifunza mengi.,.,



Mimi sipendi kukaa mjini na nadhan in the future nitahamia in the country side.,
I had a dream about My Shamba Life na kama itakuwa hivyo nitafurahi sana kwani kila kitu ni kujipanga tu maishani na pia kinawezekana kama utaamua wewe kama wewe.
Najaribu waonyesheni mengi sana through blogu yangu,kwanza lifestyle yangu ili ujue na uelewe kuwa hakuna kitu muhim maishani kwanza kama kujitambua,cha pili ni kutafuta chako kwa jasho lako,kukamilisha ndoto zako na cha tatu kujithamini na kupenda familia yako.
Hakuna kitu kitakuja kwa urahisi bali fanya maamuzi,jipange na anza kutafuta kile unataka.
Maisha sio mashindano bali tunatakiwa kukifanyia kazi kile tulichonacho kwa wakati huo.
Kumbuka kuwa wewe mwenye milioni huwezi shindana na wa billion kwani utajiumiza tu na maishani kwetu kila mmoja anamzidi mwenzake namna moja au nyengine ukishaelewa hili basi formula ya maisha haitokusumbua kichwa.

Life is truly what you make it meaning maisha ni yale wewe utakayoamua kuyaishi laasivyo itakula kwako na tamaa jamani tamaa ni mbaya maana unaweza kuta mtu anapata bahati kimaisha ila tamaa inamponza and looses everything.
Tamaa na Uwongo huwa havimfikishi mtu yoyote yule popote,kumbuka hilo.
Fake life ni kujidanganya mwenyewe na kujicheleweshea the real life ambayo umepangiwa,zingatia!
Watu husifia ujinga ili na wao for a second waone wako level moja so ukifanya vitu vya kimaendeleo usitegemee pongezi kwani midomo yao huwa mizito so wewe endelea na harakati zako as long as anayenufaika ni wewe basi simama imara kama mti wa maembe.
Sio kila mtu atakuwa Che Guevara au Barack Obama ila hiyo haimaanishi kuwa wewe huna impact kwani sometimes kuitwa mzazi bora au rafiki bora ni impact kubwa sana kwa waliokuzunguka.
Mama yetu alituambia mimi sio tajiri kwamba nikifariki ntawaachieni mali nyingi bali nataka muelewe kuwa Utajiri wenu ni umoja wenu na kupendana kwenu kama ndugu maana kama hampendani je si mtaumizana tu na hizo mali?
Kwa mliopo Nje wekezeni kwenu kwa maisha ya kesho wapendwa.,
Kuwa na malengo ni kitu kizuri na bora so fanya kazi kwa bidii,jitume,jipe moyo,kuwa jasiri,fanya maamuzi mazuri ya kimaendeleo,kuwa na subra lakin pia usisahau kuhave fun na kuwa na amani ya moyo kwani what is mali kama huna furaha na amani ya moyo.
Niseme kwa vyote lakin when it comes to kupiga kazi na kutafuta changu kwa jasho langu naomba uniheshim tena si kidogo bali sana,Nimemaliza.com!!