Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Wednesday, March 22, 2017

RESPECT MY HUSTLE CAUSE IT TAKES WORK,DEDICATION,DISCIPLINE AND WILL POWER TO TURN THE DREAM INTO REALITY!!!










 MASHALLAH YAMEKUWA VIZURI SANA.,

 Asante mungu am happy to see progress but also my hustle,,









 Mtoto nilokuwa nimembeba ni wa huyu kaka mtuwangu wa nguvu..,Mungu azidi kukuweka!
 Akinieleza mengi na kunifunza mengi.,.,



Mimi sipendi kukaa mjini na nadhan in the future nitahamia in the country side.,
I had a dream about My Shamba Life na kama itakuwa hivyo nitafurahi sana kwani kila kitu ni kujipanga tu maishani na pia kinawezekana kama utaamua wewe kama wewe.
Najaribu waonyesheni mengi sana through blogu yangu,kwanza lifestyle yangu ili ujue na uelewe kuwa hakuna kitu muhim maishani kwanza kama kujitambua,cha pili ni kutafuta chako kwa jasho lako,kukamilisha ndoto zako na cha tatu kujithamini na kupenda familia yako.
Hakuna kitu kitakuja kwa urahisi bali fanya maamuzi,jipange na anza kutafuta kile unataka.
Maisha sio mashindano bali tunatakiwa kukifanyia kazi kile tulichonacho kwa wakati huo.
Kumbuka kuwa wewe mwenye milioni huwezi shindana na wa billion kwani utajiumiza tu na maishani kwetu kila mmoja anamzidi mwenzake namna moja au nyengine ukishaelewa hili basi formula ya maisha haitokusumbua kichwa.

Life is truly what you make it meaning maisha ni yale wewe utakayoamua kuyaishi laasivyo itakula kwako na tamaa jamani tamaa ni mbaya maana unaweza kuta mtu anapata bahati kimaisha ila tamaa inamponza and looses everything.
Tamaa na Uwongo huwa havimfikishi mtu yoyote yule popote,kumbuka hilo.
Fake life ni kujidanganya mwenyewe na kujicheleweshea the real life ambayo umepangiwa,zingatia!
Watu husifia ujinga ili na wao for a second waone wako level moja so ukifanya vitu vya kimaendeleo usitegemee pongezi kwani midomo yao huwa mizito so wewe endelea na harakati zako as long as anayenufaika ni wewe basi simama imara kama mti wa maembe.
Sio kila mtu atakuwa Che Guevara au Barack Obama ila hiyo haimaanishi kuwa wewe huna impact kwani sometimes kuitwa mzazi bora au rafiki bora ni impact kubwa sana kwa waliokuzunguka.
Mama yetu alituambia mimi sio tajiri kwamba nikifariki ntawaachieni mali nyingi bali nataka muelewe kuwa Utajiri wenu ni umoja wenu na kupendana kwenu kama ndugu maana kama hampendani je si mtaumizana tu na hizo mali?
Kwa mliopo Nje wekezeni kwenu kwa maisha ya kesho wapendwa.,
Kuwa na malengo ni kitu kizuri na bora so fanya kazi kwa bidii,jitume,jipe moyo,kuwa jasiri,fanya maamuzi mazuri ya kimaendeleo,kuwa na subra lakin pia usisahau kuhave fun na kuwa na amani ya moyo kwani what is mali kama huna furaha na amani ya moyo.
Niseme kwa vyote lakin when it comes to kupiga kazi na kutafuta changu kwa jasho langu naomba uniheshim tena si kidogo bali sana,Nimemaliza.com!!

8 comments:

Anonymous said...

Oooh well done nuru, mie mwenywe Niko LA for few years, now najenga kwetu arusha mjengo WA kujitosheleza na kuweka biashara zangu sawa afterwards nikurudi arusha living a good life inshallah.

NURU THE LIGHT said...

From the bottom of my heart nakutakia kila la kheri..Ahsante if am ever in L.A hahaha tuonane!!

Anonymous said...

Nuru naomba nikuombe msamaha kwani niliongea niliyoyasikia sorry nlikutukana sana kwa sintah

Anonymous said...

i had a bad experience starting a business over there, so many hoops you have to jump to establish something .. the people in power do not help neither... But I will hopefully try again!!

Anonymous said...

Munguamweke pema peponi Sintah
Aendelee kupoteaaa.
Ingekuwa haya ya bashite nna ya madawa tusingehema kwa kumtetea Marinda.
Mungu alishakusamehe .
Hivi watz lini tutatafuta maendeleo?? Tuwafikiee hata wakenya achana na wasouth na wanigeria.
Mtu unathubutu kumchamba mtu ambaye haja wahi hata kukutusi .JIULIZE mapungufu gani unayo dah.
Mungu atubariki

Bintinyota said...

Duh!! Una dreams kama zangu and my wish ni kuishi nje ya mji full mifugo. Kishamba hapo nguvu kazi.

Nakuombea Allah akujaalie kheir utimize ndoto zako

Anonymous said...

Hongera Nuru. Nzuri sana. Hata Mimi nimependa

Anonymous said...

Nakupenda Light