Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Monday, October 10, 2016

DET HÄR ÄR INTE OK,OH DEAR HERE WE GO AGAIN!!!



Hivi lini Weusi mtajua kuithamini thamani yenu,,
Hivi lini mtajifunza kuhusu historia yenu na jinsi wenzetu walivyoteseka just because ya rangi yao,,
Inasikitisha mwaka 2016 mtu mweusi tena Muafrika anasupport ujinga huu.
This is not comedy nor Parody na mnaojifanya mnajua maana ya Parody then ningewashauri mjielimishe kuhusu hilo,,
Zamani wakati Weusi hawaonekani kwenye TV weupe walikuwa wakipaka nyuso zao na rangi Nyeusi kitu kinaitwa the black face,Google it and educate yourself.
Hata mpaka leo Youtube kama video ya msanii inacontain a black face huwa wanaitoa na hii i hope wataifuta au kuiblock,,
Sasa kama mtu mweusi anafanya hivi mweupe afanyaje?
NA akifanya mtamsema anawadhalilisha,,
When are you gonna learn?
Mimi i did not find it funny at all na Barakah japokuwa amekupa go ahead hakujua kuwa utapaka masizi na kufanya hivi ndiomaana amekumind na ni haki yake kwani nyimbo ni yake na unatengeneza hela huku ukimdhalilisha that is not ok,,
Mbona wasanii wengine hukujipaka au weusi wake ndio umeona ni target wakati wewe mwenyewe ni Muafrika mwenzake!
Hii tabia ya kuuona weusi as comedy has to stop,,
Mnawafundisha nini watoto kuhusu Kujikubali kama walivyo?
Kiasi watu wajikoboe kama mnawafanya wajihisi wana kasoro just because of the colour of their skin,,
This made me really sad na kilichoniumiza zaidi ni yeye Stanbakora kutokuelewa impact aliyonayo kuona yuko sahihi wakati he!s not!!
There is so much hurt and degrading behind a black face that it makes me sick to my stomach to see this,am done!!

3 comments:

Anonymous said...

Tatizo letu kubwa waTz huwa tunajifanya tunajua kila kitu hata vile tusivyojua badala ya kujifunza tunataka kuonekana tunajua. Na hii mitandao ya kijamii imekuwa kama pepo kila mtu anajitahidi awezavyo kutafuta umaarufu wenyewe watoto wa mjini wanakwambia KIKI. Tuwe wakweli pale mtu anapokosea tuseme amekosea sio tunatetea kila kitu. Stan Bakora ni comedian sawa hatukatai ila naona kwa kufanya alichofanya amevuka mipaka inabidi amtake radhi Baraka. Kupewa ruhusa kuiga nyimbo sio tatizo ni hayo aliyoyaongeza, baada ya Baraka kuonesha kutopendezewa na alichokifanya angekuwa mstaarabu angemtaka radhi Baraka basi yaishe. Ila sasa wapo watu wanaomponda Baraka. Kweli mama yangu alikuwa ananiambia kuwa uyaone nilijuwa ni magorofa ya posta kumbe YA WALIMWENGU...TNS

NURU THE LIGHT said...

100percent facts,,nimekupenda Tns!!

Anonymous said...

Kwa kweli sikuipenda ile video ya Stanbakora kabisa na hata watu wanavyom hatack Baraka pia nilijaribu kumtetea niliambulia vichambo kama vya buku jero hivi nakuambiwa kuwa mimi ni fake account ya Baraka. Wengine wanashadadia hata hawana point za msingi za kumtetea huyo Stanbakora na kudai kuwa Baraka kaanza kupaka sijui vipodozi ndo maana siku hizi anapendeza ila zamani alikuwa kama masizi. Ikimaanisha kuwa huwezi kuwa mzuri au kupendeza ukiwa mweusi bila kung'arisha rangi na hizo chemicals zao, so sad. Winnie