Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Friday, October 7, 2016

AHSANTE KWA TAARIFA TUNASHKURU!!!

Wazazi wa yule mtoto sijui wana hali gani,,
Yule mtoto pia sijui ana hali gani,Pole sana mdogo wangu.
Nadhani it is high time muanze kujitizama kama Watanzania kwa ukatili unaofanyika kwenye jamii na kujiita Taifa la wananchi wakarimu na wapole, ,
Kuna vitu vinafanyika vinawapasa mjiulize je hii ndio Tanzania tunayoitaka?
Tusimuongelee Scorpion au hawa walimu just because ukatili wao tumeuona na hauwezi kukatalika Bali tuongeLee Reality.
WHAT about wale wanaotesa kila kukicha watoto wa wenzao?
WHAT about wale wanaotesa kila kukicha wafanyakazi wa ndani?
WHAT about mabosi na wenye vyeo wanaowatumia kimwili wafanyakazi wao kwenye maofisi au idara mbali mbali?
Mnajua effects za kutukana watu kila kukicha mitandaoni je umejiuliza ni jinsi gani unamuumiza mwenzio au kwavile unahisi haumii basi unajiona uko better than Scorpion,,
Kosa ni kosa tu na litabaki kuwa kosa especially ukimfanyia binaadam mwenzako,,
Mimi sijashangaa kuona huyu mtoto kupigwa kwani wanawake wangapi na watoto wanapigwa kila kukicha na hamna mtu wa kuwatetea?
Wanaume wangapi wanaona wako sawa kuwadunda na kuwajeruhi wake zao?
Wazazi wangapi wanawapiga watoto wao wenyewe majumbani mwao so why is it different today,,Tafakari!
It is high time mkiona mtu hatendewi haki muungane na kupinga sio kulook the other way halafu leo mnashangaa,Really!!
Amkeni kuna watu wanafanyiwa ukatili daily vijijini ni vile tu hatuvioni,,
As a country tunataka kuozesha watoto wa kike je huo sio ukatili?
Watoto wa kike na wa kiume wanabakwa tena na family members huwa mnakaa na kukoment ushuzi leo mnashangaa mtoto kupigwa,Really
It is high time mjiulize mnataka Tanzania ya aina gani,watu wa aina gani,MAADILI na utu yapewe kipaumbele na haki itawale kwa wote not only for you but kwa watoto wenu pia.
Mungu ibariki Tanzania maana kika kukicha kuna jipya,nimemaliza.com!!!

7 comments:

Anonymous said...

kinachohitajika ni elimu elimu elimu, watu waelimishwe haki zao na asasi zisizo za kiserkali na hata kidini na huu mfumo dume uangaliwe kwa upya. Culture zina evolve na kuna watu husimama kidete mpaka mabadili fulani yatokee na kuhakikisha sheriza zinabadilishwa. Tusipoelimishana tutabakia palepale. Inashangaza sana maandiko ya dini zote yanasisitiza upendo lakini waumini sie sijui tunasoma maandiko gani tumekuwa wakandamizaji wakubwa hata hofu ya Mungu hakuna. Sita sema mengi leo ila kweli lazma watu waelimishwe hasa kujua sheria vizuri, haki zao na pia kurekebisha baadhi ya tamaduni hazifai kabisa kwa haki za binadamu. Watanzania tunajiita wakarimu na wapole kwa miaka ya karibuni tumekuwa wanyama, huku ugenini saa nyingine unaogopa kusema wewe ni mtanzania tulivyokithiri kwa mabaya...CinTea

NURU THE LIGHT said...

Umeongea point nzuri sana Cintea,,

Anonymous said...

Nuru natamani watu wakujue zaidi kwa wingi wasome maneno yako you are unique

anonymus said...

Wananchi na asasi zisizo za serikali tusimame kidete kuisaidia serikali katika mapambano dhidi ya ukatili wa aina zote..hali ni mbaya,haya tunayoyaona ni machache mengi hayaripotiwi...!

anonymus said...

Wananchi na asasi zisizo za serikali tusimame kidete kuisaidia serikali katika mapambano dhidi ya ukatili wa aina zote..hali ni mbaya,haya tunayoyaona ni machache mengi hayaripotiwi...!mwamini

Bintinyota said...

Cintea umemaliza

comfort said...

Ukatili ni mkubwa sana Tanzania ila watu hawajui haki zao.pia hata ukiijua hiyo haki utajuta kuzungushwa hasa huyo alokufanyia akiwa anapesa.lakini kama alivyosema mchangiaji wa kwanza.Elimu ndy kila kitu pia Upendo ndy kila kitu ukiwa na upendo lazima utakuwa na Huruma pia kwa binadam mwenzako.Mungu atusaidie sana atujaze Upendo huu ukatil utakwisha