Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Saturday, August 20, 2016

CASTO CHOKOZA MTU YEYOTE DUNIANI ILA SIO MWANAMKE ALIEINGIA LABOURT,TRUST YOU ME UTAJUTRAAA!!!



I LOVE YOU CASTO BUT HII STATEMENT ULIKOSEA LABDA UNGETUMIA MANENO MENGINE UNGEELEWEKA TENA VIZURI MNO,,
NIMEKUELEWA UNATAKA WA MAMA JAPO KUWA WAMEJIFUNGUA ILA BADO WA JIPENDE ILA NADHAN MANENO ULOTUMIA YALIKUWA MAKALI SANA,,
NA MWILI WA MWANAMKE HUBADILIKA SANA AKIWA MJAMZITO NA BAADA YA KUJIFUNGUA HUMUONI HATA KIM K MWENYEWE HUJIFICHA WAKATI AKIWA MJAMZITO MAANA MWILI WAKE HUFURA NA SASA NLIKUWA SIJATIZAMA PICHA ZAKE MDA AMEJIKONDESHA SANA KWAVILE KAWAONA KOURT NA KHLOE WAMEPUNGUA NA KINGINE KIM ANA WATU KAMA 100 WATAKAOWEZA KUMSAIDIA YEYE KURUDI ALIVYOKUWA,,
ANA ACCESS YA PRIVATE TRAINER,NUTRITIONIST,DIETIST,DOCTORS AND EXPERTS WA KUMSAIDIA SASA MWAJUMA ANAANZA WAPI?
KUNA VITU COMMON SENSE TU INASAIDIA KUJUA KUSEMA ILI UJUMBE WAKO UWAFIKIE WATU KWA KISTAARABU LAASIVYO UTAKULA MATUSI AMBAYO HATA HAYAKUWA NECESSARY TO BEGIN WITH,,

2 comments:

Anonymous said...

Hahahahahaha chezea kuingia labor wewe. Huyo kaka alikuwa na point ya msingi ila kwenye kuiwasilisha ndio kaharibu. Na hivi ukweli wenyewe mchungu. Ni kweli Nuru ukizaa mwili unaharibika ila ukitaka uwe kama ulivyoku mwanzo inawezekana sema wanawake wengi baada ya kuzaa huwa tunajisahau sana matokeo yake mwili unaendelee kujaa mwisho wa siku unashindwa hata kujua ufanye nini. Ulaji mzuri wa chakula, unywaji wa maji kwa wingi na kufanya mazoezi haviitaji uwe na uwezo mkubwa maana kama utaamua kula mboga za majani kwa wingi, maharage, dagaa na matunda (kutokana na msimu wake) sidhani kama ni gharama, sawa na kunywa bia kila siku. Mimi nilijifungua kwa operation nikawa na tumbo kama pipa shepu imeharibika kabisa, nilipoamua kutake action sasa hivi tumbo langu liko flat nimerudi mwili niliokuwa nao miaka 22 iliyopita. KINA MAMA TUKIAMUA KUBADILI MUONEKANO INAWEZEKANA BILA YA KUTUMIA GHARAMA KUBWA NI KUKUBALI TU KUCHANGE LIFE STYLE. Nimemaliza.com in Nuru's voice.

Anonymous said...

Casto kaenda mbali, angemtolea mfano shemela wa taifa Zari (mnyonge mnyongeni haki yake mpeni),Zari baada ya kumzaa Tiffa alijituma haswa na akaweza kurudi kama alivyokuwa mwanzo, yaani ukiambiwa ana watoto wanne huwezi amini na ndio maana anazaa kila kukicha kwa maana kuzaa kwake sio tatizo akishazaa muonekano unarudi kama alivyokuwa mwanzo. Badala ya kumnyeshea Casto mvua ya matusi tungejifunza kitu, yawezekana amewasilisha manung'uniko ya wanaume wengi tu wa kitanzania wakiwemo waume zetu pia.