Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Sunday, January 31, 2016

UJUMBE MZURI SANA JANECCY,I HOPE THEY LISTEN!!!



Vijana Wenzangu Tanzania 
There's a lesson we should learn . Somo kuu Sana . Hakuna kinachoniuma Sana Kila nikifungua simu na kukuta vijana wanafariki Hasa kwa ajali . Tena ajali zenyewe ni Zile za magari binafsi na Bodaboda . Paul Walker , lost his life on car accident and we mourned but there was a reason for search incident . A message to be delivered to all car/motorcycle lovers and owners . Tuwe makini barabarani . Watu wengi wanapoteza maisha kwa uzembe wao au wa watu wengine wanaotumia barabara. Najua yafuatayo ; magari ni kipimo cha mafanikio yetu na Bodaboda pia ni chanzo cha mapato ama usafiri nafuu kwetu Ila pia ni mtego wa ujana wetu . Mara nyingi tunaendesha mwendo kasi , hatufungi mikanda , tunaendesha tukichat ama tukiongea na simu , wengine wakiwa na ulevi na hata wale wanaokatazwa kuendesha magari kutokana na sababu za kitabibu huwa nao wanaendesha . Bado sasa Bodaboda , Yani ukiona mbwembwe za vijana wanaoendesha Bodaboda unaweza ukaumwa . Basi Kama hauamini katembelee MOI au Sewa Haji pale Muhimbili. Yani hali ni mbaya mno mno . Ifike mahali tusambaze na kupaza Sauti zetu juu ya usalama wa barabarani lakini pia kuendesha kwa umakini. Dar Es Salaam mji Mkuu Una ajali nyingi Sana ambazo zimesababisha Vifo . Nimepoteza rafiki zangu wengi vijana kwa ajali za papo hapo na nyingi zimesababishwa na wenyewe . Nimeshuhudia majeruhi wa ajali hizi wakiwa kwenye maumivu makali . Sisi tuliopo hai tuna wajibu wa kuwalinda wengine dhidi ya ajali hizi. Asikuambie mtu , hamna maumivu makali Kama mzazi anapompoteza Mwana tena Mwana kijana . Tuwe mabalozi wenyewe wa usalama barabarani. Kama hatutaambizana ukweli , tutakwisha tu . Kwa Maana wengi kipimo cha mafanikio cha kwanza ni kununua gari . Sio kitu kibaya Kuwa na usafiri wako Ila ni mbaya Sana kuruhusu usafiri huo ukatize ndoto zako . Tusambaze ujumbe . Mimi Kama mbunge kijana nimeona tuna wajibu wa kukumbushana kuhusu usalama barabarani ‪#‎KijanaMtanzania‬ ‪#‎EndeshaKwaUsalama‬ ™

GONE TO SOON CALVIN DUE TO A CAR ACCIDENT,,REST IN PEACE!!!

No comments: