Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Sunday, November 1, 2015

KUNA AMBAO WALISHANIOMBA MSAMAHA NA KUNA AMBAO BADO NASUBIRI WANIOMBE MSAMAHA,THE CHOICE IS YOURS!!



Dada mmoja alikuwa airport akisubiri connetion ya ndege yake, wakatangaziwa ndege itachelewa saa mbili zaidi.
Akaamua kununua gazeti na box Dogo la biscuits, akatafuta sehemu akakaa kusoma gazeti kusubiri muda ufike wa kuingia kwenye ndege, alipokaa pembeni yake kulikuwa na kaka nae anasoma gazeti akisubiri ndege. Dada alishangaa alipokuwa akitoa biscuit kwenye box aliloliweka pembeni yule kaka nae anachukua moja anakula, akamwangalia kwa hasira, kaka akawa anatabasamu.
Dada akakasirika akataka kumtolea maneno machafu akajizuia. Ukawa mchezo kila dada akichomoa biscuit moja yule kaka nae anachukua moja. Ikaendelea hadi ikabakia biscuit moja.
Yule kaka akawahi kuichukua akaimega nusu akampa yule dada, ...dada kwa ghadhabu akanyanyuka akamtukana sana yule kaka na maneno ya kumdhalilisha kwanini anavamia vitu vya watu asinunue vyake!! Kaka alikaa kimya bila kumjibu yule dada.
Mara wakatangaziwa muda wa kuingia kwenye ndege umefika. yule dada akaingia akimuacha kaka nae akisubiri ndege yake.
Alipokaa kwenye siti yake akafungua mkoba aweke simu yake, mara alishtuka kuona box lake la biscuits zima wala halijafunguliwa, kumbe alikuwa anakula biscuits za yule kaka. Akajutia sana akatokwa na machoz jinsi alivyomdhalilisha yule kaka, na muda wa kurudi kuomba msamaha haupo tena kwani milango ya ndege ilishafungwa na kuanza kuondoka.
"Muda wa kuomba msamaha kwa uliyemkosea upo usisubiri milango ifungwe"...
Kiburi, wivu, husuda ni sifa za Ibilisi.
Nawatakia jumapili njema nyooote! Kama umemkosea mtu, umemsingizia ili aonekane mbaya au ukimsema huku ukijua sio kweli unachosema au ukimharibia mtu maisha, wahi kumuomba msamaha kabla milango haijafungwa🙏🏽⏰⌚🕗
UKIIPENDA SHARE TAFADHALI KAMA NILIVYOFANYA MIMI!

No comments: