Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Tuesday, July 28, 2015

CURRENT SITUATION,NITARUDI!!!




NASHKURU SANA RIPOTA WANGU MAANA MPAKA WATU WANADHANI NIKO NCHINI NA HIZI UPDATES KUMBE NIKO ÄLVSJÖ,,,,



4 comments:

Anonymous said...

Picha ya pili kutokea chini, nikimuangalia mke wa Lowasa naona bado hayuko comfortable, bado kuna mashaka makubwa ndani yake. Lakini yote sio kitu cha ajabu kwa sababu huyu mama ana marafiki zake mashosti wake wake wenziwe wa viongozi huko alikotoka ghafla bin vuu anajikuta yuko mwenyewe na watu wengine wapya inabidi aanze upya socialization, aanze upya kutengeneza base yake. Kwa kweli aliyescrifice hapo sehemu kubwa ni huyo mama, Mzee Lowasa yeye anahamia huko na marafiki zake ukute ndio waliomshauri, bado ataendelea kupata support na kuhang out na wenziwe lakini mama wa watu atabaki kuwa mpweke, labda support ya ndugu na jamaa. Uzuri nduguze wengi na mashemeji wako UKAWA toka zamani, atazoea tu.

Issue inakuja kwa kurisk huko je atabakia kupata zile huduma alizokuwa anapata kama Waziri Mkuu Mstaafu kutoka serikalini?

Na je akikosa hiyo nafasi ya urais anayoigombea kupitia Ukawa, Chadema watampa nafasi ya kuwa Mwenyekiti wa Chama au hata nafasi yoyote kubwa katika Chama? Au itakuwaje mwanawane? I hope wamekwishakubaliana hivyo vitu kwa maandishi maana kina Tundu Lissu hawakawii kumgeuka tena baada ya kumtumia wakati uchaguzi.

Sie yetu macho na masikio lakini kusema ukweli Chadema wao ndio walisimama kidedea kumharibia sana safari yake hiyo ya Urais na mara ya mwisho walisema wazi kuwa CCM ikimsimamisha Lowasa wao wataenda Mahakamani na huku wanamsema kuwa Fisadi mpaka alipokatwa na CCM. Sasa sijui upepo na mtazamo wao umebadilishwa na nini au ndio Chungu kaona ganda la muwa?

Im just thinking aloud, kwa kweli nilikuwa nawaamini kiasi fulani wapinzani kuwa walikuwa wanasema kweli lakini kwa hili mmh kumbe ni mambo ya siasa tu ya kuharibiana. Nishajiandikisha kadi yangu ninao nafikiri itabidi nibadilishe uelekeo kura yangu ya Urais nampa Magufuli hata kama CCM siipendi na Magufuli simpendi lakini angalau ana msimamo.

Anonymous said...

Haya na wengine waliokatwa kina Membe, Makamu wa Rais Dr. Bilal na Mzee Pinda nao wanahamia wapi? Au wao kukatwa kwao hakujawauma sana kama kulivyomuuma Lowasa au wao wana vyeo vidogo kuliko yeye?

Kura yangu hapati ng'ooo ngoja akaliwe mpaka senti yako ya mwisho huko UKAWA halafu atawaponza CDM wasipewe tena msaada na chama cha Conservative cha UK kama wanavyopewa miaka yote kwa sababu uliwafukuza wale wazungu wa maji kutoka UK, pia aliwafukuza wazungu wa kampuni ya serikali ya UK mwaka ulee. Subiri tu wazungu ndio watawakomesha hawa kwa kuwanyima hizo pesa wanazoringia.

Anonymous said...

Hii siasa jamani ina mambo mengi sana sawa na michezo ya kuigiza michafu jamani.

Anonymous said...

Membe haitajiki ukawa. He has nothing to offer. Ukawa wanahitaji substance sio smile ya mtu.