Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Monday, May 4, 2015

MASOUD KIPANYA SAID!!!




Kwa mara ya kwanza kabisa katika
maisha yangu najuta kabisa kuwa
mtanzania, taifa la watu wajinga,
taifa lisilo na mbele wala nyuma,
jambo ambalo hata mtoto mdogo
haliwezi kumsumbua eti majitu
mazima yanapiga yowe kuwa dola
imepanda. Mnataka shilingi ya
Tanzania ipande kwenda wapi?
Wasomi gani nyie msiojua uchumi?
Sh ya Tanzania ipande kwa lipi?
Mnazalisha nini hapa Tanzania ili
kuinua uchumi?
Kila kitu watanzania mnanunua nje
ya nchi, wewe unayesoma hapa
hebu jikague umevaa mavazi ya
wapi? Kuanzia viatu, suruali,
chupi,soksi, shati hadi saa vyote ni
nje ya nchi, magari yote, pikipiki
na vipuri ni nje ya nchi hadi
sindano, stick za meno na sukari
mnaagiza nje, wakulima wa
machungwa Muheza wanakufa njaa
nyie mnaagiza machungwa kutoka
South africa na juice kutoka Kenya,
taifa gani hili? More imports than
exports halafu eti shilingi ipande,
watanzania mnapenda kuishi
kimiujiza kuliko uhalisia, ndio
maana wengi wenu ni washirikina
wa kutupwa, viwanda mmeua
halafu shilingi ipande, tena ngoja
sasa hivi dola moja itakuwa sh
5,000 tuone mtafanyaje......?
CHUKUA HATUA HAPO ULIPO

1 comment:

Anonymous said...

well said, otherwise tutondoka nchini kabisa maana tumechoka sasa