Genuine Nordic Vodka

Genuine Nordic Vodka

Saturday, August 30, 2014

MPAKA DAMU YA MTU IMEMWAGIKA NDIO MUELEWE MAANA YA CYBERBULLYING,IS THIS WHAT YOU HAVE BECOME AS A NATION!!


LEO WAKATI NAINGIA FACEBOOK KITU CHA KWANZA KABISA KUKUTANA NACHO NI HII MAKALA KUHUSU BETTY,,BAADA YA KUISOMA NIKASEMA MAYBE NOW WATU WATAELEWA MADHARA YA CYBERBULLYING NA INASKITISHA KUWA KIFO CHA MTU NDO KIWE MFANO KWANINI LAKINI,,
YAANI HILI NDIO TAIFA LA KUJIVUNIA KUWA HIVI NDIVYO TUMEKUWA KWELI??JE HUYU ANGEKUWA MTOTO WAKO,AU NDUGU SASA HIVI UNAJISKIAJE WAKATI NA WEWE PIA NI FOLLOWER WA MAPAGE KIBAO HUKO INSTANGRAM,,AMKENI NA MBADILIKE HUYU NI MTOTO SANA KUPOTEZA MAISHA YAKE KIUKATILI HIVI,REST IN PEACE BETTY NDEJEMBI!!
kapumzike kwa amani na uwasemehe walioshindwa kukuface na kukwambia kama umewaudhi bali wakachukua hatua nyengine na kufanya ukatili
jamani msifikiri kila mtu yuko strong binadamu tunatofautiana istoshe huyu dada akuwa na wazazi na sometimes wazazi wetu plays a big part kwenye maisha yetu,,yaani kaniuma huyu mtoto utadhani namjua but haina haja kiubinadamu WE FAILED YOU BETTY,,



Ninaandika makala hii nikitambua bayana kuwa itamuudhi kila mtu anayeingia mtandaoni kwa minajili ya kuwanyanyasa wengine. Lakini siku zote ninaamini katika busara hii: kuuchukia ukweli hakubadilishi ukweli kuwa uongo. Ukweli ni ukweli na uongo ni uongo. Ukweli hauwezi kuwa uongo, na kadhalika uongo hauwezi kuwa ukweli. Kamwe asilani.

Wakati tunaomboleza kifo cha ndugu yetu Betty Ndejembi watu wamesema mengi, na yameandikwa mengi. Kila mmoja kwa namna alivyoguswa. Zitto Kabwe ametweet hivi asubuhi "Justice for Betty", akitoa rai haki ipatikane kwenye kifo cha Betty.
Jokate Mwegelo nae ametweet kuomba msaada wa kuchunguza kifo cha Betty. Na watu wengine maarufu kila mmoja kasema neno, labda kwa sababu Betty alikua maarufu in one way or another.
Lakini hatuwezi kukwepa ukweli kwamba siku chache kabla ya kifo chake, alinyanyaswa mno kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter. Japo hadi muda huu hatuwezi kuhusisha moja kwa moja uhusiano kati ya unyanyasaji huo na kifo chake, lakini mtu akinyanyaswa masaa kadhaa kabla ya kifo chake, waweza kujenga picha flani.
Saa chache kabla ya kifo chake Betty alitweet kua "PINDA HAWEZI KUWA RAIS". Baada ya kutweet hakuonekana tena hadi alipookotwa mtaroni kesho yake asubuhi akiwa amefanyia vitendo vya kikatili na akiwa amepoteza fahamu.
Lakini kabla hata ya kutweet hivyo, Betty alikua anaandamwa sana mtandaoni huko Twitter. Kuna watu walianzisha team ya kumtukana, kumjibu hovyo na kumprovoke kwa kila alilofanya.
Naomba ieleweke kuwa simlaumu mtu kwa sababu sina mamlaka ya kufanya hivyo bali dhima ya makala hii ni rambirambi zangu kwa Betty kuzungumzia tatizo la unyanyasaji mtandaoni, sambamba na suala zima la unafiki kila kinapojiri kifo hususani cha mtu maarufu.
Tuna tatizo kubwa huko mitandaoni. Tumefika hatua ya kuwapa umaarufu watu wenye matusi ya nguoni, wazushi, wambeya, wanafiki. Wanaochafua wenzao, kutishia wenzao kwa kujifanya askari JKT, kusengenya na kupost majungu.... Aina ya binaadamu wanaostahili laana lakini twaishia kuwatukuza.
Kwenye hii mitandao, matusi imekuwa njia ya mkato ya kupata umaarufu. Kuna wenzetu wengi tu wenye 'umaarufu' huko Twitter, Facebook na Instagram lakini ukidadisi chanzo cha 'umaarufu' huo, utaambiwa 'ah huyu ana matusi si mchezo!'
Kuna watu wazima na akili zao wanatumia muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii aidha kunyanyasa wenzao kama si kusherehesha unyanyasaji huo.
Marehemu Betty ni victim wa yote hayo. Alitukanwa sana, na aliitwa majina kadhaa ya kumdhihaki kabla ya kukutana na mauti. Kuna waliomwita Di Maria, superstar uchwara etc.. and i hope hao waliomuita hivyo wanajifahamu na wengine wananisoma hapa.
Japo sijui chanzo cha 'ugomvi' wao, lakini naamini kuna watu wengi tu waliokuwa 
katika nafasi ya kuzima moto huo kwa vile walikuwa wakizifahamu pande zote mbili za 'ugomvi' husika lakini kwa sababu ya unafiki wakapalilia moto maana wanafurahi watu wakigombana.
La kukera zaidi ambalo ni wazi litajichomoza wakati wa maombolezo haya ni UNAFIKI. Watu walewale waliodiriki kumwandama marehemu wakati wa uhai wake watageuka kuwa wenye uchungu mkubwa baada ya kifo chake. 
Hii inanikumbusha suala ambalo nimeshawahi kulizungumzia mara kadhaa kwamba 'wakati muafaka wa kutafuta vipaji vya uigizaji ni kwenye misiba: watu walewale waliokuwa wakikuchukia kwa nguvu zote watageuka wenye uchungu mkubwa kwa kifo chako.'
Ukiangalia baadhi ya tweets za mwisho za marehemu ni wazi kuwa binti huyo alikuwa anahitaji msaada kutoka kwa wanaomjali.
Mojawapo ya Tweet za mwishomwisho za marehemu alisema hivi "Do I have a sister to support me? No. Do I have a Dad/Mom to run to or support me. No. Im hurting and wanna cry? Yes. BUT I know God is watching"
Haihitaji degree ya Saikolojia kujua kuwa Betty alikua kwenye kipindi kigumu mno na alihitaji msaada kwa watu waliokua karibu yake. 
Betty anauliza"Nina dada wa kunisaidia? Hapana. Nina baba au mama wa kumkimbilia? Hapana. Nimeumizwa/nina uchungu na ninahitaji kulia (lakini nitamlilia nani?). Ila najua Mungu anaona"
Kwa bahati mbaya Betty hakuwa na baba, hakuwa na mama, hakuwa na dada wala kaka. Wote walishatangulia mbele ya haki. Alibaki peke yake, peke yake na Mungu wake.
Lakini binadamu wasivyo na aibu wala huruma wakazidi kumtukana na kumsimanga, huku wengine wakiporomosha matusi mazito. Hawakujua yaliyokua moyoni mwake. Wakamtambia kwa maisha mazuri wanayoishi na namna walivyobarikiwa.
Betty akiwa katika maumivu makali ya hisia akapost hivi "Thank you all for the names i was called, luck y'all have such a perfect life.! No hard feelings.. Im alive still.! Endeleeni kuongea"
Kwa tafsiri isiyo rasmi Betty alisema "Asanteni kwa majina yote mliyoniita. Mmebarikiwa kuwa na maisha mazuri.! Hamuumizwi na hisia kama mimi. Ila bado ninaishi, endeleeni kuongea"
Kwa bahati mbaya hakuna aliyejali, hadi juzi asubuhi (jumatano) Betty alipookotwa kwenye mtaro akiwa amefanyiwa unyanyasaji wa kijinsia na akiwa amepoteza fahamu.
Kifo cha Betty ni miongoni mwa vifo vya kikatili sana kuwahi kutokea nchini. Nashauri wanaharakati ea haki za wanawake wapambane kuhakikisha haki inapatikana. Akina Annanilea Nkya, Hellen Kijobisimba watafute haki ya binti huyu kzma Zitto Kabwe alivyosema "Justice for Betty"
Imagine mtu aliyekua kwenye maumivu makali ya hisia, anatekwa na genge la wahuni. Bila kujali kipindi kigumu alichokua anapitia, bila kujali hakua na wazazi, bila kujali psychological toacher aliyokua nayo still wanamfanyia unyanyasaji wa kijinsia hadi anapoteza fahamu.
Betty aliokotwa mtaroni na kupelekwa hospitali. Jana (alhamisi) aliweza kufungua macho, lakini hakuweza kuongea lolote hadi saa 3 usiku wa kuamkia leo, mauti ilipomkuta.
Kwaheri Betty, kwaheri classmate wangu (Majengo sec), kwaheri rafiki, kwaheri ndugu. Umeondoka dunia bado inakuhitaji. Naumia u have gone too young, lakini naumia zaidi coz umekufa kikatili mmno. Japo sijui nitakufaje, lakini nadiriki kusema hukustahili kifo cha aina hii.
Nakumbuka sms yako ya mwisho kwangu uliniambia hivi "Malisa blv me, only youths can change this country". Leo nilipopata taarifa ya kifo chako nimerudia kuisoma sms yako mara mbilimbili. Sikujua kua sms hiyo ndo ulikua unaniaga. 
Umeniaga kwa kutuachia vijana wosia, kuwa vijana pekee ndio wenye uwezo wa kuibadilisha nchi hii. Nitakua nimekusaliti ikiwa sitautendea kazi wosia huu. I promise to fight and motivate other youths to liberate this country for ur dedication.
Umekwenda kumfuata mama yako, umemfuata baba yako. Wazazi wako walitangulia, leo wewe umewafuata. Hatimaye familia nzima mmekutana Paradiso.. Pumzika kwa amani Betty.!

12 comments:

Anonymous said...

cyber bullying na physical assault,alikutwa jumatano mikocheni kapigwa na kubakwa yani ni mdogo sana hakustahili mateso yote hayo

Anonymous said...

we will miss her...and may she travel safe.
but da nuru i think you are incorrect when you speak on cyber bullying regarding Tanzania.
now do not think i am condoning it, i never said you were wrong to speak on it. but if you look at America, they bring awareness to the issue, they have organisation, support groups online and offline, the use the media, they have rallys, some of the states are starting to formulate and implement laws on all kinds of bullying, they show the full scale of the problem and the consequences.
people in Tz think all is a game, and kufikiri nikimsema mtu labda atatoka tu on social networks and that is the worst that could happen. i think it is time we bring this issue to light in Tanzania and it should be vocalised quite loudly, i hope my opinion does not disturb you. i was quite sad when i heard the news and was talking to an acquaintance and this is when all this hit me, she said things like, kwani ulimjua kabisa, kwani si angetoka tu humo mitandaoni, it really upset me to the point i think i've cut her off..
man, i hate bullys, especially online 'gangsters',

Disminder orig baby said...

niko na nyie nyote jamani instagram kumezidi na huko kungine kote.

yaani watu wamekuwa na mamlaka ya juu zaidi kwa maisha ya watu why?

aaaah mimi uwa sisifiii mtu pasiposifika na wala simtukani mtu but namwambia ukweli tu.

unahisi mtu kakukwaza basi mwite chemba mwambie. hivi hata kama hajakusikia ukikaa kimya unapungungukiwa nini?
na ulivyosema huko umepata nini?

kwa kweli inabidi tubadirike sana.
Watanzania tumevamia vitu kwa haraka sana. tumeharibu maana ya urahisi wa mawasiliano haya.

kwa nini tusisambaze habari njema?
kwa nini tusitangaze biashara tukaongeza kipato?
yes mtangazie mtu mwambie akupe commission yako kwa kuwa una followers wengi. you get they get maisha yanaendelea kila mmoja akifaidika.

Vipi kesho Mwenyezi Mungu atatuhukumu? mimi pia jana nimeumia sana, sikutaka hata kuendelea kuangalia news.

Allah atampa wepesi, na tunaomba sana amsamehe makosa yake. Amin

Anonymous said...
This comment has been removed by a blog administrator.
Anonymous said...

May her soul rest in eternal place...for a hundred time I'm not regretting not having any social medias page and I know it's easy for communication with others but it's very sad how many abuses and turn it into war zone. This breaks my heart but God will give her true justice to those who were involved in this.

Anonymous said...

Sionagi sababu yakugombana na mtu kwenye mitandao ukiona mtu anakushambulia jibu ni kukaa kimya ndio jibu la mjinga ilo sasa ukitaka kubishana ndio tatizo huanzia huko. ..naomba kuuliza kitu mauaji yake yamethibitishwa sababu ni hiyo?

Anonymous said...

daah jamani its sad kuona mtoto mdogo hivyo anapoteza maisha kisa mitandao. kwani ni lazma mtu awe na hayo na sijui twitter,ID NA upuuzi mwingine?haya mambo yanasikitisha sana

NURU THE LIGHT said...



MDAU WA MWISHO TATIZO SIO KUWA NA BLOG,TWITTER,INSTA,FB OR WATEVA TATIZO NI UTUMIAJI MPENZI,,

Anonymous said...
This comment has been removed by a blog administrator.
NURU THE LIGHT said...


UKIWEKA OPENLY WHO YOU ARE NA KUMTAJA UNAYETAKA MWAMBIA KINACHOKUUDHI NITARUSHA KOMENT YAKO,,
KAMA TUNATAKA HIVI VITU VIISHE WE HAVE TO START DEMANDING MABADILIKO LAASIVYO TUNAKUWA HATUNA TOFAUTI YA KUJIFICA NYUMA YA ANONYMOUS,,
KAMA KUNA MTU ANA BLOG,PAGE O WEBSITE UNAMUONA ANA BULLY WATU CHUKUENI ACTIONS MBONA NJIA ZIPO WARIPOTINI TUU BUT MKITAJA MAJINA YA WATU BEHIND ANONYS THEN U JUST BECOME THAT KUMBUKENI KAMA WADAU MNA POWER KUBWA SANA MBONA MWENZENU NIMEWEZA KUBLOG MDA WOTE HUU BILA MAJUNGU NI KUWA NA MSIMAMO TUU HATA KINA FLANI WAKIKUCHOKOZA MAANA MWISHO WA SIKU I KNOW THE TRUTH AND I KNOW WHO I AM,,ONE LOVE

Anonymous said...

Ha ha haaaa Nuru ntakutandika kibao weweee, umeiminya comment yangu, mie sijamtaja mtu jina, kwa nini ajishtukie. Au unamwogopa Nuru? Keh keh keh keh. I understand u my dada, potezea tusonge mbele. Ila siku nitamchomea nishapajua pa kumchoma. Namsubiria tu abully mtu.

NURU THE LIGHT said...


hahhaha ntandike tuuu mamiii,,ucjali nimekuelewa,,